Pre GE2025 Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Simiyu Ashiriki Mkutano Mkuu wa Jimbo la Maswa Mashariki

Pre GE2025 Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Simiyu Ashiriki Mkutano Mkuu wa Jimbo la Maswa Mashariki

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)

Stephano Mgendanyi

JF-Expert Member
Joined
May 16, 2020
Posts
2,833
Reaction score
1,301

Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Simiyu Ashiriki Mkutano Mkuu wa Jimbo la Maswa Mashariki

Maswa, 16 Januari 2025 – Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Mkoa wa Simiyu, Ndugu Shemsa Mohamed Seif, ameshiriki Mkutano Mkuu wa Jimbo la Maswa Mashariki uliofanyika katika Uwanja wa Ngunzo Nane, Maswa. Mkutano huu umefanyika kwa ajili ya kusoma na kujadili utekelezaji wa miradi ya maendeleo katika Jimbo hilo, linaloongozwa na Mbunge, Mhe. Stanslaus Nyongo.

Mgeni rasmi katika mkutano huo alikuwa Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Kassim Majaliwa Majaliwa, ambaye aliwaeleza wananchi hatua kubwa zilizopigwa katika kuboresha huduma za kijamii na miundombinu ndani ya Jimbo la Maswa Mashariki.

Akizungumza katika mkutano huo, Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Simiyu, Ndugu Shemsa Mohamed Seif, alimpongeza Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, kwa kuendelea kuwekeza katika maendeleo ya Mkoa wa Simiyu. Alieleza kuwa katika kipindi cha 2020-2025, Serikali imewekeza zaidi ya Shilingi Bilioni 78 katika miradi mbalimbali ya maendeleo ndani ya Jimbo la Maswa Mashariki pekee.

Mwenyekiti huyo pia alisisitiza kuwa Chama na Serikali mkoani Simiyu vinafanya kazi kwa ushirikiano wa karibu ili kuhakikisha wananchi wanapata maendeleo na huduma bora zinazostahili.

Imetolewa na: Idara ya Siasa na Uenezi,
Chama Cha Mapinduzi (CCM) – Mkoa wa Simiyu
 

Attachments

  • WhatsApp Image 2025-02-16 at 21.34.30.jpeg
    WhatsApp Image 2025-02-16 at 21.34.30.jpeg
    380.3 KB · Views: 1
  • WhatsApp Image 2025-02-16 at 21.35.53.jpeg
    WhatsApp Image 2025-02-16 at 21.35.53.jpeg
    181.9 KB · Views: 1
  • WhatsApp Image 2025-02-16 at 21.35.29.jpeg
    WhatsApp Image 2025-02-16 at 21.35.29.jpeg
    377.2 KB · Views: 2
  • WhatsApp Image 2025-02-16 at 21.35.13.jpeg
    WhatsApp Image 2025-02-16 at 21.35.13.jpeg
    169.8 KB · Views: 1
  • WhatsApp Image 2025-02-16 at 21.35.11.jpeg
    WhatsApp Image 2025-02-16 at 21.35.11.jpeg
    496.9 KB · Views: 1
  • WhatsApp Image 2025-02-16 at 21.35.06.jpeg
    WhatsApp Image 2025-02-16 at 21.35.06.jpeg
    392.7 KB · Views: 2
  • WhatsApp Image 2025-02-16 at 21.35.04.jpeg
    WhatsApp Image 2025-02-16 at 21.35.04.jpeg
    459.5 KB · Views: 3
  • WhatsApp Image 2025-02-16 at 21.34.42.jpeg
    WhatsApp Image 2025-02-16 at 21.34.42.jpeg
    554.3 KB · Views: 2
  • WhatsApp Image 2025-02-16 at 21.34.32.jpeg
    WhatsApp Image 2025-02-16 at 21.34.32.jpeg
    310 KB · Views: 1
Hilo jimbo nadhani ni kati ya majimbo masikini sababu ya kukumbatia CCM, wakitoka hapo watapewa pombe na nyama ndiyo malipo yao.
 
Back
Top Bottom