Mwenyekiti wa CHADEMA Vijana Kanda ya Nyassa, Victor Baleke, amekamatwa na kuwekwa ndani katika Kituo cha Polisi Rujewa asubuhi hii. Baleke alihojiwa jana katika Kituo cha Polisi Chimala na alipewa dhamana.
Taratibu za kufuatilia dhamana nyingine zinaendelea. Aidha, kuna taarifa zinazoonyesha kuwa Mwenyekiti wa CCM Wilaya ya Mbarali, John, pamoja na mtoto wake, ndiyo wanashinikiza vijana wa CHADEMA wawekwe ndani.