Mindyou
JF-Expert Member
- Sep 2, 2024
- 1,869
- 4,877
Wanabodi,
Mwenyekiti wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi, Jaji Jacobs Mwambegele, amesisitiza kuwa kujiandikisha zaidi ya mara moja ni kosa la jinai lenye adhabu ya kifungo cha angalau miezi sita, kisichozidi miaka miwili, au vyote kwa pamoja.
Ameyasema haya wakati wa mkutano na wadau wa uchaguzi mkoani Tanga, ulioshirikisha viongozi wa serikali, vyama vya siasa, taasisi, dini, na kimila. Vituo vya uandikishaji vitafunguliwa saa 2 asubuhi na kufungwa saa 12 jioni.
Zoezi la uandikishaji wa daftari la wapiga kura litaanza Februari 13 mwaka huu katika mikoa ya Tanga na Pwani na litadumu kwa siku saba.
Source: East Africa Radio
Mwenyekiti wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi, Jaji Jacobs Mwambegele, amesisitiza kuwa kujiandikisha zaidi ya mara moja ni kosa la jinai lenye adhabu ya kifungo cha angalau miezi sita, kisichozidi miaka miwili, au vyote kwa pamoja.
Ameyasema haya wakati wa mkutano na wadau wa uchaguzi mkoani Tanga, ulioshirikisha viongozi wa serikali, vyama vya siasa, taasisi, dini, na kimila. Vituo vya uandikishaji vitafunguliwa saa 2 asubuhi na kufungwa saa 12 jioni.
Zoezi la uandikishaji wa daftari la wapiga kura litaanza Februari 13 mwaka huu katika mikoa ya Tanga na Pwani na litadumu kwa siku saba.