Mindyou
JF-Expert Member
- Sep 2, 2024
- 1,869
- 4,877
Jumuiya ya Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM) Mkoa wa Dodoma umewataka Wananchi wa Wilaya ya Mpwapwa mkoani Dodoma kuwaogopa Viongozi wanatokana na vyama vya upinzani akiwemo Mwenyekiti wa BAVICHA Taifa kwa kuwa watu hao siyo salama na wasioitakia mema nchi ya Tanzania.
Kauli hiyo imetolewa na Mwenyekiti wa UVCCM Mkoa wa Dodoma Abdulhabib Mwanyemba katika mwendelezo wa ziara yake na Kamati ya Utekelezaji ya Umoja huo ya Wilaya na Mkoa Wilayani Mpwapwa walipotembea Shule ya Sekondari Fuime na Matomondo, kuzindua shina tawi Mpwapwa Mjini Katika Mtaa wa Mazae Kati, Tambi Shule na Kizimkazi pamoja na NHC.
"Kuna wenzetu wale wa upande wa pili na niseme tu kwa uwazi. Imetoa mwenyekiti wa BAVICHA Taifa na kuna vikao vya siri wanakaa, wamejipanga kuja kugombea bunge la Mpwapwa lakini wanajipanga kutengeneza wagombea wa nafasi za udiwani katika kata zilizopo hapa Mpwampwa"
Lakini mkumbuke huyu kiongozi wa BAVICHA Taifa ni mbunge wa kamati kuu ya CHADEMA ambaye mwenyekiti wa CHADEMA anasema No reforms no election. Hawa ni watu ambao hawaitakii mema nchi yetu ya Tanzania kwa hiyo tuwe makini na tusije tukasikiliza mambo ambayo wanayaleta. Hawa watu sio watu salama kwa nchi yetu."
Kauli hiyo imetolewa na Mwenyekiti wa UVCCM Mkoa wa Dodoma Abdulhabib Mwanyemba katika mwendelezo wa ziara yake na Kamati ya Utekelezaji ya Umoja huo ya Wilaya na Mkoa Wilayani Mpwapwa walipotembea Shule ya Sekondari Fuime na Matomondo, kuzindua shina tawi Mpwapwa Mjini Katika Mtaa wa Mazae Kati, Tambi Shule na Kizimkazi pamoja na NHC.
"Kuna wenzetu wale wa upande wa pili na niseme tu kwa uwazi. Imetoa mwenyekiti wa BAVICHA Taifa na kuna vikao vya siri wanakaa, wamejipanga kuja kugombea bunge la Mpwapwa lakini wanajipanga kutengeneza wagombea wa nafasi za udiwani katika kata zilizopo hapa Mpwampwa"
Lakini mkumbuke huyu kiongozi wa BAVICHA Taifa ni mbunge wa kamati kuu ya CHADEMA ambaye mwenyekiti wa CHADEMA anasema No reforms no election. Hawa ni watu ambao hawaitakii mema nchi yetu ya Tanzania kwa hiyo tuwe makini na tusije tukasikiliza mambo ambayo wanayaleta. Hawa watu sio watu salama kwa nchi yetu."