Mwenzangu umefanikiwa vipi biashara ya kuuza Duka?

Mwenzangu umefanikiwa vipi biashara ya kuuza Duka?

Majigo

JF-Expert Member
Joined
Feb 23, 2012
Posts
5,519
Reaction score
1,828
Ni miaka miwili sasa, najitahidi angalau nione manufaa, hatimaye ijiendeshe na kuinua maisha yangu na jamii yangu.
Lakini sasa naona inanishinda hata kuaibika kwani Biashara haiendelei na nazidi kushuka kiuchumi

Sijui nakosea wapi machief?

Asante

Jigo
 
biashara ya duka mara nyingi mtaji wake ni mdogo mdogo ila kama biashara ndogov za nyumban
 
Ni kosmetics mkuu, sio biashara Ya Nyumbani

Unaisimamia wewe, manunuzi wewe, kuuza wewe, kufanya hesabu wewe!!! Miaka miwili hujagundua ni tatizo gani linakufanya usiendelee?? Inawezekana biashara yako ni sawa na kuuza barafu Ueskimoni ambapo barafu kwao ni kero.

Toka ulipo tafuta eneo jingine la biashara. Mafuuuuuuuuuuuuuuuuuuu!
 
Naungana na mdau hapo juu kuhusu muda wa Biashara kufikia miaka miwili na kuona inashuka.Hapo kuna tatizo

Kwanza Lazima tukujue Tabia yako.
Maana hata mlevi ukimkuta Bar atakuambia hajalewa ila yeye amepita tu hapo kajikuta anayumba.

Biashara nyingi hizi huwa zinachangamoto nyingi
-Kwanza ni kiashiria kizuuuri sana cha madem,ukihonga hata lips stick basi jua umejimaliza mwenywe
-Lugha,mara nyingi wenye mali,huona kwamba wao ndio kila kitu hasa siku za mwanzo wa biashara,sasa inawezekana kwamba uliharibi tangu mwanzo na umeshindwa ku pick tena.
-Kuna uptodate,kwenye matoleo ya bidhaa,sasa sijui kama unaenda na wakati huo.

Sasa kama kuna moja kati ya hayo,fanya madiliko,moja ikiwemo tafuta mtu umuajiri kwa miezi sita uone nini kitatokea.
sio kila mwenye biashara anaweza kuwa muuzaji mzuri.Ku deal na kinadada inataka moyo saana,na ukikera tu basi wanatabia ya kususa kwa muda mrefu,na wakiambizana ndio kifo chako cha biashara.

We angalie wale chinga wanaopaka madada rangi za kucha,yaani akienda kwenye kijiwe basi wanaambizana huyu jamaa yupo vizuri basi anaunganisha kazi hapo hapo.

La ziada tathmini Location yako.
 
Chonde chonde usianze kwenda kwa waganga maana hamchelewi, zingatia ushauri wa wadau, au kuna maduka mangapi yenye bidhaa kama zako hapo?
 
sio wewe pekee, dola imepanda,uchumi umekuwa mgumu,watu hela za vipodozi wamepunguza.

sekta zinazolipa kwa sasa ni zile zisizoepukika kama usafirishaji kwa dar,biashara ya vitoweo kama samaki au mboga mboga na vyakula kwa bei nafuu. kwingine wengi wanaumia sana kipindi hiki. shukuru Mungu kukaa miaka 2, wengine hufilisika ndani ya miezi 3.
 
Back
Top Bottom