condorezaraisi
JF-Expert Member
- Sep 4, 2011
- 225
- 116
Poleni sana na huu msiba mkubwa uliotupa wana JF
Naomba msaada wenu kimawazo, Nimeolewa na nina watoto wawili...Mtoto wangu wa kwanza wa kiume nilimzaa nikiwa form two ,nikamrudisha home kwa bibi yake akipata matunzo na mie kuendelea na masomo mpaka hapa nilipofikia katika umri na kazi yangu hii,
Tangu nimezaa mtoto yule sikuwahi kupata matumizi yoyote toka kwa baba yake ingawa kwetu alipafahamu vyema..nimemtunza kwa taabu sana huku nikisaidiwa na wazazi wangu.
Mpaka pale nilipopata kazi na mme ambaye alichukua majukumu ya kumtunza mtoto kama wake.
Leo hii mtoto wangu kamaliza darasa la saba. Mara nikaanza kupokea msg nikiulizwa mtoto wangu kafaulu mwez Dec sikujibu ? nikajua tu huyu sasa atakuwa baba wa mtoto kaanza kujileta..zileendelea kuingia msg mfululizo ambazo nilikaa kimya .
Baada ya kuona imekuwa kero na hizo msg ndipo nikaona nimpigie simu na kumwambia ndio mtoto amefaulu na baba yake anamtafutia shule nzuri ili ampeleke, Yakaanza kuporomoshwa matusi
Ooh mtoto wangu ushamu- adopt nakumpa baba mwingine ,Naona wewe mwanamke ni mpumbavu sana unajifanya una ndoa eeh ,kuna baba mwingine zaidi yake ,umeona nimeshindwa kumsomesha mtoto wangu,tena naanza taratibu za kumfata mwanangu na nitatafuta namba ya huyo mmeo nimwambie akae akijua huyu sie mwanaye ni mwanangu mie
Nilibaki nimepigwa butwaa huku nimeshikilia simu na kukosa la kumjibu ...kwani sikutegemea maneno kama hayo at that time
Baada ya hapo akaendelea kutuma msg za kashifa sikujibu msg hata moja ila nimebakia nawaza sina hata jibu mie mtoto alishaenda shule.
Jamani nimfanyeje huyu mtu wa kuanza kunitukana bila kosa..
NB: Namba zangu alizipata pale alipopiga simu kazini kwetu nikiwa nimesafiri sijui alisema nini mpaka akapewa namba zangu,
Naomba msaada wenu kimawazo, Nimeolewa na nina watoto wawili...Mtoto wangu wa kwanza wa kiume nilimzaa nikiwa form two ,nikamrudisha home kwa bibi yake akipata matunzo na mie kuendelea na masomo mpaka hapa nilipofikia katika umri na kazi yangu hii,
Tangu nimezaa mtoto yule sikuwahi kupata matumizi yoyote toka kwa baba yake ingawa kwetu alipafahamu vyema..nimemtunza kwa taabu sana huku nikisaidiwa na wazazi wangu.
Mpaka pale nilipopata kazi na mme ambaye alichukua majukumu ya kumtunza mtoto kama wake.
Leo hii mtoto wangu kamaliza darasa la saba. Mara nikaanza kupokea msg nikiulizwa mtoto wangu kafaulu mwez Dec sikujibu ? nikajua tu huyu sasa atakuwa baba wa mtoto kaanza kujileta..zileendelea kuingia msg mfululizo ambazo nilikaa kimya .
Baada ya kuona imekuwa kero na hizo msg ndipo nikaona nimpigie simu na kumwambia ndio mtoto amefaulu na baba yake anamtafutia shule nzuri ili ampeleke, Yakaanza kuporomoshwa matusi
Ooh mtoto wangu ushamu- adopt nakumpa baba mwingine ,Naona wewe mwanamke ni mpumbavu sana unajifanya una ndoa eeh ,kuna baba mwingine zaidi yake ,umeona nimeshindwa kumsomesha mtoto wangu,tena naanza taratibu za kumfata mwanangu na nitatafuta namba ya huyo mmeo nimwambie akae akijua huyu sie mwanaye ni mwanangu mie
Nilibaki nimepigwa butwaa huku nimeshikilia simu na kukosa la kumjibu ...kwani sikutegemea maneno kama hayo at that time
Baada ya hapo akaendelea kutuma msg za kashifa sikujibu msg hata moja ila nimebakia nawaza sina hata jibu mie mtoto alishaenda shule.
Jamani nimfanyeje huyu mtu wa kuanza kunitukana bila kosa..
NB: Namba zangu alizipata pale alipopiga simu kazini kwetu nikiwa nimesafiri sijui alisema nini mpaka akapewa namba zangu,