sikujua dada FF unaroho mbaya namna hii ,wewe ni mama na kama hayakukuta kwa wanao basi yatakukuta kwa wajuuu,haya mama siku njema na imani wewe ni msafi siku zote, nawashukuru wengine wote waliojitolea kunishauri hawana uchoyo wa msaada kwani mpaka sasa nimeshapata mwanga
liwe fundisho kwa wanawake wote kuwa ukishazaa na mwanaume ukae ukijua ata apote baadae either baba au mtoto mwenye atataka kumjua mtoto au baba yake...hivyo mkiwa mwanasa mimba mlijuwage hilo sio mwajiachia tuu
Watu wengine badala ya kushauri wanahukumu,nyie ni wasafi sana enhe.Kosa husamehewa, kosa ni kurudia kosa.Dada C,mshirikishe mumeo,na kama baba wa mtoto yuko tayari kumsomesha mwanae,mumruhusu,mtoto ana haki ya kumjua na kuhudumiwa na baba yake.
Wewe unielewe mimi!!!!!Hii inaonesha ukomavu wako. Asante kwa kutusaidia kukuelewa ni wa aina gani.
Wazazi kama walikusamehe sawa na mtoto wako ana kosa gani asimjue baba yake.asante fazaa kama makosa nilishafanya na wazazi wangu walinisamehe na kunipokea na bado wakaendelea kunipa elimu,hapa nilihitaji ushauri zaidi ,anyway nashukuru kwa mtizamo wako pia
Ofcourse zinaa ni dhambi!
Lakini hakuna dhambi isiyosamehewa!? Lazima turudishe moyo nyuma na kusamehe wenzetu. Othewise dunia haitakuwa mahali pazuri pa kuishi! Iman yangu inaweza kutofautiana na yako ie mzinzi apigwe mawe hadi afe lakini asiye na dhambi na awe wa kwanza kumtupia mawe!
Ni hayo tu!
FF, mhusika amekubali ya kuwa amekosa, sidhani kama huu ni muda wa kumponda mwenzetu ambaye yupo njia panda, kwani maji yalishamwagika!!! Shida yake ni ushauri tu ambao utaweza kumsaidia kwa sasa.