Mwezi ukilipuliwa kwa bomu la nuclear, nini kitatokea?

Hapa ndipo huwa natambua fikra na uelewa wa baadhi ya watanzania. Kadri miaka inavyokwenda ndivyo waathirika wa akili na vipofu wa mioyo wanavyoongezeka!
Hali hii inasababishwa na ulaji kemikali na chanjo zilizozuiwa mataifa yalioendelea.
 
Hapa ndipo huwa natambua fikra na uelewa wa baadhi ya watanzania. Kadri miaka inavyokwenda ndivyo waathirika wa akili na vipofu wa mioyo wanavyoongezeka!
Hali hii inasababishwa na ulaji kemikali na chanjo zilizozuiwa mataifa yalioendelea.

If you take JF too serious you will end up get madness
 
Leo nimeona limwezi likubwa sana ni kahisi lina ka siku mbili limeonekena
 
Mdau - thanks for thinking. Hata mimi huwa nawaza mawazo haya mazito. Over the years nimegundua kwamba tabia hii imenifanya niwe mdadisi zaidi hata katika mambo ya kawaida na niko informed sana. Kiufupi ni kwamba hakuna bomu la Nyukia lenye nguvu kwa sasa linaloweza kuleta madhara makubwa kwa mwezi. Kwa sasa ukipiga kibomu chako cha Nyuklia, inawezekana huku duniani wala tusijue what is going on. Kimbembe ni pale ikitokea another big heavenly body igongane na mwezi na kufanikiwa kuumega mega au kuusambaratisha kabisa.

Kama heavenly body kubwa ikifanikiwa kuusambaratisha mwezi kabisa, miamba michache ya mwezi inaweza kupenya na kutudondokea hapa duniani. Hatari zaidi hata hivyo itatokana na kutokuwepo kwa mwezi wenyewe. Bila mwezi maisha yetu hapa duniani yatakoma. Mwezi unai-stabilize dunia na kuifanya ibakie katika njia yake bila kutetereka. Hili ni jambo la muhimu sana katika maisha yetu hapa duniani kwani dunia ikisogea kidogo tu mbele au nyuma basi jua linaweza kutuletea matatizo ama kwa joto hapa duniani kuwa kali sana au tunaweza ku-freeze permanently. Yote haya yanaweza ku-disrupt Photosynthesis, na bila Photosynthesis inamaanisha hakuna chakula na hivyo kifo kwa wengi wetu.

Bila mwezi wa kui-stabilize dunia yetu pia dunia inaweza kuongeza au kupunguza spidi yake. Wanasayansi pia wanasema kwamba without the moon, the Earth will start to wobble on its own axis utadhani mlevi wa viroba. Yote haya mawili siyo mambo mema kwani yanaweza kuingilia mfumo wa majira na kuufanya mfumo mzima uparaganyike. Jambo la hatari hata hivyo ni kwamba mambo haya yanaweza kusababisha Magnetic Field ya dunia kufifia sana na kuacha atmosphere yetu ikiwa wazi tu. Kumbuka kuwa Magnetic Field ya dunia ndiyo inatulinda na radiation na kufanya dunia yetu iwe na atmosphere. Bila magnetic field yenye nguvu radiation kutoka kwenye jua (hasa wakati wake wa plasma eruption) itaweza kudhuru viumbe hapa duniani (mbali na kukaanga grid zetu za umeme permanently). Kibaya zaidi ni kwamba bila ulinzi wa kutosha tunaopewa na magnetic field ya dunia, radiation kutoka kwenye jua inaweza kutafuna atmosphere yetu kabisa. Na hili likitokea then it is the end of the game. That means there is no Hydrological Cycle na hewa kama tulivyozoea. Life as we know it will end on this planet!


Japo tunaudharau na tunaukumbuka tu pale unapotumulikia usiku, kufanya bahari zetu kupwa na kujaa na kutufanya tule pilau wakati wa Eid, mwezi una umuhimu mkubwa sana katika mfumo mzima unaoifanya dunia yetu kuwa makazi ya mabilioni ya viumbe hai tukiwemo sisi wenyewe. We owe our very existence to the moon!
 
Hii ni sawa kujadili ujinga maana kujadili kisichowezekana, mbona hufikilii sayari ya dunia kulipuliwa?
 
Hapa ndipo huwa natambua fikra na uelewa wa baadhi ya watanzania. Kadri miaka inavyokwenda ndivyo waathirika wa akili na vipofu wa mioyo wanavyoongezeka!
Hali hii inasababishwa na ulaji kemikali na chanjo zilizozuiwa mataifa yalioendelea.

Ni kweli kaka hizi ni fikra za bange, mtu alie sawa hawezi waza lisilowezekana. kuna siku ataleta sayari ya dunia, ikilpuliwa nini kitatokea.
 
Ni kweli kaka hizi ni fikra za bange, mtu alie sawa hawezi waza lisilowezekana. kuna siku ataleta sayari ya dunia, ikilpuliwa nini kitatokea.

Please fikra msiziwekee mipaka. Ugunduzi mwingi hapa duniani umetokana na watu kuwaza mambo yasiyowezekana. This might look far fetched lakini hata leo hii mwezi unaweza kugongana na other heavenly body na ukasambaratishwa. This is a real possibility. Hili likitokea dunia itapona?

Wakati huu tunapoongea NASA wana kitengo maalum cha wataalamu ambao hawalali na kazi yao kubwa ni ku-scan universe ili kuona kama kuna mjiwe huko unatujia. Na kama upo one of the theory ni kuufuata huko huko na kuutwanga mabomu ya Nyuklia ama kuuvunja vunja au kuu-boom ili hatimaye uweze kubadilisha trajectory na kui-miss dunia yetu.

Sasa nyie eti mnakandia bila kujua kuwa hii ina practical implication kwani huko nyuma ilishawahi kutokea na kuwamaliza akina dinosaur na 98% ya living species..

Please acheni fikra za watu zichanue hata kama ni katika mambo yanayoonekana kuwa ni too abstract/useless. YOU NEVER KNOW!!!
 
Mwezi ni mdogo kwa ukubwa ukilinganisha na dunia

Mwezi una size gani ukilinganisha na dunia!

Mwezi wa dunia yetu ni mkubwa kushinda miezi mingine katika-mfumo wa jua. Hakuna jina tofauti kuliko "mwezi" isipokuwa watu wametumia neno la-Kilatini-"luna" kwa ajili ya mwezi wakitaja mwezi wetu ili kuutofautihsa na miezi ya sayari nyingine.

Huwa tunaangalia uso wake upande mmoja tene uleule tu. Sababu yake ni ya kwamba siku ya mwezi ni sawa na kipindi cha mwezi duniani. Mwezi unazunguka kwenye kipenyo chake katika muda wa siku 27.321 661 za dunia. Upande wa nyuma wa mwezi uko gizani wakati sisi tunaona mwezi mpevu. Wakati kwetu mwezi hauonekani upande wa nyuma unapokea nuru ya jua.

Uso wa mwezi unajaa mashimo ya-kasokoyaliyosababishwa kwa kugongwa nameteoridi. Mwezi hauna angahewa inayozuia mapigo ya meteoridi ndogo au kupunguzu nguvu yao jinsi ilivyo duniani.
 
Wanawake watapunguza root za kwenda huko.hawapapendi sema tu ndo hvyo hajapatikana Osama wa hiyo kitu
 
Deep and analytical comment..! Tunashukuru kwa ufafanuzi murua kabisa..!
 

umeelezea vizuri...
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…