Mwigulu mnachowafanyia Singida United si sawa!

MAKULUGA

JF-Expert Member
Joined
Jan 21, 2011
Posts
7,828
Reaction score
10,527
Pamoja na kushangilia Ubingwa wa Simba kinyonge( kwa kuchukulia mikononi mwa watoto wa nyumbani) naomba kuwaonya Mh.Mwigulu kuhusu namna wanavyoifanyia Timu .!

Awali niwapongeze vijana ambao jana walijitolea kupambana na Timu kubwa yenye wachezaji Bora na utulivu wa akili na moyo kutokana na ufadhili wa Mo.

Haikuwa kazi rahisi ndio maana hata magoli mliyofungwa yalikuwa sio ya move nzuri kivile! Ingawaje hayalingani na yale (sio yote)magoli ya yaliiwezesha Yanga kushika nafasi ya pili kwa maajabu!

Si mnakumbuka magoli mengine walikuwa wanafunga kwa mgongo ,makalio nk!

Mheshimiwa Mwigulu ,nini kimewapata hadi kufikia vijana wanakosa chakula ,nimeshangazwa jana kambini hali haikuwa nzuri ,wengine hata pa kula walikuwa hawajui.

Hiyo pesa mliyokuwa mnaitoa awali mliipata wapi hadi inafikia hatua hii.Jana kuna vijana wanatishia kugomea kwenda Tanga.

Cha kushangaza bado Sanga anajinadi kuwa Singida bado ipo imara.

Kwa hali hii ,huko mbele ni giza!

Au Mheshimiwa ndio hiki kinachosemwa mtaani kuwa 2020 ulitaka kuhamia Singida Mjini,kukimbia move ya 'lombo kumweli' kule nyumbani! [emoji2957] ... Lakini nako upepo hausomi!!??.
 
Huyu mwigulu si ndiye aliewagawia yanga wachezaji wa singida
 
Singida united ni yanga b..itakosaje njaa!
 
Majuzi hukumbuki kuna timu moja ligi kuu iliwajaza wachezaji wote kwenye land cruiser, hawana hata basi wala costa
Km kweli wanakosa chakula bora ishuke daraja hawajui thamani yao
 
Mwigulu Nchemba kama timu ya mpira tuu imekushinda kuiongoza urais ungeuweza kweli???singida united ni timu iliyopata bahati ya kuwa na wafadhili wengi
 
Singida United iliharibiwa na siasa, Mo alikuwa mdhamini, halafu mwenyekiti Mwingulu hataki wachezaji wauzwe kwingine zaidi ya kuuziwa yanga, basi Mo ikajitoa
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…