SAYVILLE
JF-Expert Member
- Mar 25, 2010
- 7,895
- 12,975
Siyo mpenzi sana wa kufuatilia wala kuongelea maisha binafsi ya mtu ila hili naomba nitoe kama angalizo kwa muhusika tajwa ila inaweza kufaidisha na wengine.
Mwijaku amekuwa na tabia ya kupost video akiwa huko ughaibuni. Nakumbuka video zake kule Ivory Coast kwenye AFCON kama kumbukumbu zangu zipo sahihi. Kama sikosei niliwahi ona video yake nyingine kule Uarabuni kama sikosei na kuna hii nimeiona jana au juzi akiwa huko Marekani.
Katika video hizi zote, Mwijaku anaonekana akitembea kwa miguu barabarani katika hali inayohatarisha maisha yake na watumiaji wengine wa barabara. Wenzetu wana sheria za "jaywalking" ambayo inahusiana na kutembea au kuvuka barabara bila kufuata sheria. Ile video ya Mwijaku akiwa Marekani ni "jaywalking" moja kwa moja na watu huwa wanakamatwa na kushtakiwa kwa kosa hilo.
Sehemu kama Marekani ambapo kupata viza ni kimbembe, anaweza kutokea hater mmoja akaforward video zake kwa wakulungwa akapigwa pini asikanyage tena huko.
Holaaa.
PS. Sina ukaribu naye ila ningekuwa nao ningemtumia huu ujumbe katika mawasiliano yake binafsi.
Mwijaku amekuwa na tabia ya kupost video akiwa huko ughaibuni. Nakumbuka video zake kule Ivory Coast kwenye AFCON kama kumbukumbu zangu zipo sahihi. Kama sikosei niliwahi ona video yake nyingine kule Uarabuni kama sikosei na kuna hii nimeiona jana au juzi akiwa huko Marekani.
Katika video hizi zote, Mwijaku anaonekana akitembea kwa miguu barabarani katika hali inayohatarisha maisha yake na watumiaji wengine wa barabara. Wenzetu wana sheria za "jaywalking" ambayo inahusiana na kutembea au kuvuka barabara bila kufuata sheria. Ile video ya Mwijaku akiwa Marekani ni "jaywalking" moja kwa moja na watu huwa wanakamatwa na kushtakiwa kwa kosa hilo.
Sehemu kama Marekani ambapo kupata viza ni kimbembe, anaweza kutokea hater mmoja akaforward video zake kwa wakulungwa akapigwa pini asikanyage tena huko.
Holaaa.
PS. Sina ukaribu naye ila ningekuwa nao ningemtumia huu ujumbe katika mawasiliano yake binafsi.