Mwinyi Zahera amkataa Kakolanya Yanga

dos santos

JF-Expert Member
Joined
Nov 22, 2010
Posts
256
Reaction score
128
Kocha wa timu ya Yanga Mwinyi Zahera amemkataa kipa Beno Kakolanya na kwamba ameruhusu aendfe timu nyingine na si Yanga.

Akizungumza na Yanga TV Zahera amesema wale waliomwambia aache kufanya mazoezi wamtafutie timu kabla ya dirisha la usajili kufungwa ila kwa Yanga haiwezekani tena.

Kama ilikuwa ni kutingisha kibiriti, kwa mkongo huyu kimejaa. Nidhamu kwake ndio jambo la kwanza kwa mchezaji. Misimamo yake na kwa mpira wetu wa bongo huenda wachache wakamuelwa.
 
Safi sana. Atakuja kwetu Msimbazi
 
Mwinyi Zahera halijui soka la Tanzania viongozi na mashabiki kwa Sasa watamuunga mkono kwasababu Yanga wanapata matokeo Kila msimamo wake ataonekana kocha Bora.
Siku Yanga watakapo Anza kupoteza mechi hata amini atakachokiona watamgeuka pale jangwani na watamfurusha na viboko wakiongoza na mzee Akilimali. Simba na Yanga hazijui vizuri huyu.
Unamuacha kakolanya unategemea Kabwili hadi mwisho wa msimu?
 

Kwa upande mwingine uko sahihi kwamba matokeo yakianza kuwa hasi kwa Yanga upepo utabadilika...lakini hii ni kwa dunia nzima kwani hii ndiyo saikolojia ya mashabiki wote wa soka duniani..lakini kwa ujumla wake kocha Zahera yuko sahihi kabisa.Huwezi kumkaribisha mchezaji aliyegoma..kwani mwenye matatizo ya kucheleweshewa malipo siyo Beno peke yake...wachezaji kadhaa wa Yanga wana madai yao...sasa Beno alifanya hivyo kwa kuwa alivimbishwa kichwa yeye ndiye kipa bora kwa Yanga na kwamba ni lazima atingishe kiberiti kwa kugoma...ni jambo baya sana...yaani waandishi wa habari wanaowadai mishahara kadhaa waajiri wao wagome kwenda kazini!!! Halafu wafanyakazi wa taasisi za ummawenye madai yao wagome kwenda kazini...haiwezekani...alichofanya Kakolanya ni upuuzi wa kiwango cha juu...hisia zangu zinanituma niamini kuwa Beno alishawishiwa afanye hivyo na meneja wake ambaye ni kiongozi wa Simba kwa lengo la kuihujumu Yanga...Yanga kamwe wasikubali Beno arudi Yanga, aende huko huko ikibidi aende Simba...Yanga mwaka 1976 iliwahi kufukuza wachezaji wote wa kikosi cha kwanza na kuanza upya, mwaka 1977 ilifunggwa 6-0 na Simba lakini Yanga haikufa moyo....iliendelea kujijenga na mwaka 1981 Yanga ikajikomboa kwa kuichapa Simba goli 1-0 kwa bao la Juma Mkambi.....
 
Sina tatizo na Beno kutokurudi Yanga shida je Nani anaziba nafasi yake?
Unaleta kiburi wakati njaa inauma na msosi unauona
 
Watapewa kipa wa bure na African Lyon au Singida United
Sina tatizo na Beno kutokurudi Yanga shida je Nani anaziba nafasi yake?
Unaleta kiburi wakati njaa inauma na msosi unauona
 
Reactions: Tui
Kabwili atachukua nafasi yake..madhara ya kurudi huyo Beno ni makubwa kuliko akiendelea kuwa nje ya timu...
Mnataka kumbebesha dogo zigo la lawama siku atakayofanya makosa mashabiki wa Yanga watakavyomshukia na ukizingatia umri wake mtamuua kabisa confidence yake.
Kabwili Hana uwezo wake kubimili mechi za Azam na Simba
 
Yanga wapate Matokeo wasipate Matokeo Zahera yuko asilimia 100 sahihi hatutaki mambo ya Yanga Bwanga Sisi (Nafikiri wote mnaikumbuka vizuri ile issue ya Yanga Bwanga na kilichotokea)
 
Kabwili atachukua nafasi yake..madhara ya kurudi huyo Beno ni makubwa kuliko akiendelea kuwa nje ya timu...
Kabwili atakapokuwa majeruhi, hakutakuwa na mbadala zaidi ya Kindoki
 
Mnataka kumbebesha dogo zigo la lawama siku atakayofanya makosa mashabiki wa Yanga watakavyomshukia na ukizingatia umri wake mtamuua kabisa confidence yake.
Kabwili Hana uwezo wake kubimili mechi za Azam na Simba

Uwezo anao...hata Kindoki anao uwezo...ni afadhali hao kuliko huyo msaliti Beno...hujui madhara atakayoleta kwenye timu...hivi unadhani wachezaji wenzake wanampenda huyo Beno..fanya utafiti uone...akirudi wanaweza wakafanya makusudi ili afungwe mabao mengi kuondoa kiburi chake...mabeki wanaweza wakaaamua kumfungisha makusudi..
 
Kabwili atakapokuwa majeruhi, hakutakuwa na mbadala zaidi ya Kindoki

Ndugu yangu nadhani wewe huifahamu Yanga vizuri....Akiumwa Kabwili Kindoki atadaka...upo wakati Ivo Mapunda na Shdrack Nsajigwa waligoma kuichezea Yanga na Yanga ikawafungia miezi sita...Wakati wanagoma Yanga ilikuwa haina kipa mwingine kwani walikuwa wanaumwa...Yanga ilikuwa inakwenda Arusha kucheza mechi ya Ligi dhidi ya timu ya mtu yukle alikuwa anaitwa Askofu...Ivo na Nsajigwa walitoroka kambini Morogoro na ikabidi huko Arusha akae golini Gulla Joshua ambaye alikuwa ni fowadi...Yanga ilicheza vizuri na kutoka sare ile mechi...Nsajigwa na Ivo wakafungiwa miezi sita. baada ya miezi miwili hivi akina Ivo na Nsajigwa wakaanza kufanya lobbying kwa Maximo kocha wa Taifa Stars ili wafunguliwe kuichezea Bara kwenye michuano ya Challenji...Suala likafika mpaka Ikulu lakini Yanga ikaendelea na msimamo mpaka Ivo na Nsajigwa wakamaliza adhabu ya miezi sita...Upo wakati miaka ya nyuma Yanga ilibaki na kipa mmoja tu aitwaye Fungo na ambaye alidaka mpaka Yanga ikachukua ubingwa...Yanga huwa haibembelezi wachezaji...Huyo Beno kama anataka aende huko Simba lakini Yanga kamwe hawezi 'kurudi'...ni traitor...ni msaliti...hajielewi...anatumiwa na maadui wa Yanga...aende huko anakotaka kwenda, na nakuthibitishia jambo moja nalo ni kwamba huo ndio mwisho wa mpira wake ...hawezi kucheza na kudumu miezi sita...aende tu, aone kilichowahi kuwapata wachezaji wenine waliowahi kuisaliti na kuidengulia Yanga ..
 
Heko kocha Zahara.Usajiri bwerere wa Kakolanya unanukia Msimbazi.

Yaani kocha bwege lilitaka Beno acheze tu huku familia ina njaa,watoto wanarudishwa hawana karo ya shule?Hata Ronaldo au Messi wanaweza kugoma usipowapa salary,huyo Neymar ndo usiseme kabisa.
 
Yanga wapate Matokeo wasipate Matokeo Zahera yuko asilimia 100 sahihi hatutaki mambo ya Yanga Bwanga Sisi (Nafikiri wote mnaikumbuka vizuri ile issue ya Yanga Bwanga na kilichotokea)
Uko sahihi Mkuu.....dah ilikuwa ni shiidah
 
Mchukueni mkuu
 
hamna namna sasa.
 
Kocha yupo sahihi kwa 100% kabla Beno hajaondoka alipaswa kumwambia Kocha wake nini anataka kufanya!!
Hata kurudi kwake ingekua rahisi zaidi sasa maamuzi yake ya kujiondokea yamemponza
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…