Kocha wa timu anaweza kuwa msemaje wa timu hasa kwenye maswala yanayo husiana na uchezaji wa timu (mbinu, wachezaji, na ufundi) hata timu za ulaya maswala yote yanahusu ndani ya uwanja anaongea kocha. Kwenye ishu ya Zahera kuonekana sana kwenye magazeti na tv umemlinganisha na Haji Manara, kwa mtazamo wangu naona kwavile tu waandishi wengi wa habari wanapenda kumuhoji. Je mfano ungelikuwa wewe ni kocha halafu kila wakati waandishi wa habari wanakufuata kukuuliza uliza maswali kuhusu mchezo wako au kuhusu uwezo wa wachezaji wako je ungekaa tu kimya?