Li ngunda ngali
JF-Expert Member
- Jun 22, 2023
- 707
- 2,572
Hatimaye, zama za mbabe wa siasa za jirani zetu pale Kenya bwana Raila Odinga, dalili zote zinaashilia zi-ukingoni.
Kwa namna Rais Ruto anavyotaka kushughulika na mwamba yule, hakika, ni suala la mda kwa aina ya siasa alizozizoea kufanya ili matakwa yake yatimizwe-kwa msimamo wa Dk Ruto kutokutaka hayo yatimizwe, hakika, zama za Raila zinaenda kutamatishwa rasmi.
Raila, alizoea kila baada ya kushindwa uchaguzi, huanzisha vurugu ili aweze kumsababishia ubabaifu aliye shika hatamu, aweze kumwita wakae mezani na wagawane madaraka kwa kile kilichozoea kuitwa maridhiano ya hongo. Jambo hilo Dk Ruto, amelikataa!
Bwana Odinga, hivi karibuni, ameendeleza desturi ileile huenda kwa matarajio yaleyale ya yeye kutaka apewe hongo ya hand-shake na ionekane waliopo madarakani, wanamwabudu.
Lakini, kwa namna Ruto na msaidizi wake walivyo shikilia msimamo wao wa abadani hakutakuwa na hand-shake na Odinga, ni wazi zama za Raila zinaelekea kukoma.
Pamoja na rabsha za hapa na pale za maandamano ya hivi karibuni, lakini, zipo dalili Wakenya watamchoka Raila kwa wao kutokuona Serikali ya Ruto kubabaishwa na wanachokifanya na kushikiria kiburi na ndiposa wataona bora waendelee na kutafuta shilingi ya kuwafanya wapate chochote kitu na ndipo anguko la Raila litajiri/li.
Nionavyo, zama za Raila zipo ukingoni.
Kwa namna Rais Ruto anavyotaka kushughulika na mwamba yule, hakika, ni suala la mda kwa aina ya siasa alizozizoea kufanya ili matakwa yake yatimizwe-kwa msimamo wa Dk Ruto kutokutaka hayo yatimizwe, hakika, zama za Raila zinaenda kutamatishwa rasmi.
Raila, alizoea kila baada ya kushindwa uchaguzi, huanzisha vurugu ili aweze kumsababishia ubabaifu aliye shika hatamu, aweze kumwita wakae mezani na wagawane madaraka kwa kile kilichozoea kuitwa maridhiano ya hongo. Jambo hilo Dk Ruto, amelikataa!
Bwana Odinga, hivi karibuni, ameendeleza desturi ileile huenda kwa matarajio yaleyale ya yeye kutaka apewe hongo ya hand-shake na ionekane waliopo madarakani, wanamwabudu.
Lakini, kwa namna Ruto na msaidizi wake walivyo shikilia msimamo wao wa abadani hakutakuwa na hand-shake na Odinga, ni wazi zama za Raila zinaelekea kukoma.
Pamoja na rabsha za hapa na pale za maandamano ya hivi karibuni, lakini, zipo dalili Wakenya watamchoka Raila kwa wao kutokuona Serikali ya Ruto kubabaishwa na wanachokifanya na kushikiria kiburi na ndiposa wataona bora waendelee na kutafuta shilingi ya kuwafanya wapate chochote kitu na ndipo anguko la Raila litajiri/li.
Nionavyo, zama za Raila zipo ukingoni.