mkuu hata kama ametoka kwa ajili ya kufuata pesa bado itabidi aonyeshe juhudi ili aweze kupata zaidi na ndipo huyo mtoa pesa atakuwa namcontrol anavyotaka na kumfanya mwanamke amdharau mmewe kwa vile kule anaona ana ziada apatayo
Yuko rafiki yangu alikuwa kijogoo sana wa wake za watu......... nilifanya kazi sana kumrekebisha, maana la sivyo sidhani kama angekuwa hai leo hii. Aliwahi kunisimulia kwamba, siku moja alikuwa na mke wa mtu, ambaye alimwambia kuwa ameamua kutoka nje ya ndoa ili kumkomoa mumewe, baada ya kumfumania mara mbili na ma-house girl...............(Mara nyingi wanawake hutoka nje ili kulipa kisasi)
Siku moja baada ya kufanya mapenzi, walianza kupiga stori pale kitandani............. yule jamaa yangu akamuuliza............. "hivi wewe na mumeo huwa mnafanya tendo la ndoa mpaka kufikia mshindo kama inavyotokea ukiwa na mimi?"..............Swali la kijinga eh!
Alichofanya yule mwanamke ni kunyanyuka na kuvaa na kisha kuondoka zake............... baadae jamaa alipokea ujumbe kwenye simu yake ya mkononi kwa namba asiyoifahamu ikisema............. "mie kutembea na wewe sio kwamba simpendi mume wangu, ukweli ni kwamba nampenda sana, kwa hiyo usijione mshindi, nilifanya hivyo kwa ajili ya kupunguza maumivu ya kihisia, na kuanzia leo tusijuane mshamba wewe........."
Ilimchukua muda kidogo, jamaa yangu kujua ule ujumbe umetoka kwa nani...........
sasa hapo mkuu huyo mama atakuwa amemkomoa mwanaume au atakuwa amejidhalilisha kwa jamaa
Sema tu mkuu................. au nimekukumbusha ile habari ya Blackberry! LOL
Zamani wakati nilipokuwa mtoto, ilikuwa ni aibu kubwa mtu kuambiwa amefumaniwa. Kama ni vijijini, wapiga ngoma wa kijijjini wakiongozwa na Manju wao walitunga nyimbo kuzungumzia jambo hilo. Kufanya mapenzi kiholela, iwe mjini au vijijini, lilikuwa ni jambo linalotazamwa kwa jicho la bezo.
Leo hii, kujamiiana kunachukuliwa kama moja ya burudani muhimu sana. Kwa hiyo watu kutoka nje ya ndoa zao, ni jambo ambalo linafanyika kama kwamba, ni sifa muhimu sana. Siku hizi mtu anaweza kufanya jambo hilo na yeyote, mradi tu amepata nafasi ndogo ya kujificha.
Labda hata wewe unaweza kushangazwa na jambo hili, kuna wakati mwanaume anaanza uhusiano wa kimwili na mke wa mtu, huku akijua hilo ni kosa. Lakini baadae mwanaume huyo huanza wivu kwa mwanaume halali wa mke husika . Ajabu eh!.............. Je unadhani huyu mwizi ni kichaa? Hapana, inakuwa hivyo na ndio maana watu hufumaniwa!
Wataalamu wa saikolojia wanasema, kwa mfano, mtu anapofikia mshindo wakati wa tendo, anakuwa ameingia kwenye ukaribu wa kiwango cha juu na mtu aliyeshiriki naye tendo. Baada ya tendo hilo choyo huanza, na hapo muhusika anaanza kuingia kwenye hofu ya kuachwa na hivyo anajikuta akitaka kudhibiti mienendo ya huyo mke wa mtu, jambo ambalo linaweza kupelekea kufumaniwa kwa urahisi Kwa hiyo ukiingia kwenye uhusiano na wake za watu, basi ujue ipo siku utafumaniwa tu
hii ishu iko complex mno....
sometimes unaambiwa wanawake wanatoka nje kwa sababu
nje ya ndoa kuna sex ya kutoheshimiana sana na kuogopana...
which means yale unayofikiri ukimfanyia mkeo unamdhalilisha kumbe
ndo anakwenda kuyatafuta nje.....
wazee walisema ukimheshimu mkeo,huzai nae......sio utani...
Umenena vyema lakini je itawezekana maana kila uchao matatizo haya huongezeka.Labda tufanye maombezi kwa taifa zimaMi nadhani kinachotakiwa ni m2 kuwa tu mwaminifu na kuachana na mambo ya kulipa kisasi,elewa kitu kimoja penzi ni kikohozi kuficha huliwezi utajidanganya tu!na ndio maana lazima kufumaniwa au kuhiswa na baadhi ya watu au marafiki au familia zinawazunguka jambo la msingi kuiba haifai acha!
Utu tutautoa wapi na tushakuwa wanyamaNafikiri chanzo kikubwa sana cha watu kufanya haya mambo ni kukosa UTU na kutokuwa na HURUMA na watu wenye ndoa zao. Tuuvae ubinadamu, halafu tuwe na UTU ndugu zangu .....
sasa hapo mkuu huyo mama atakuwa amemkomoa mwanaume au atakuwa amejidhalilisha kwa jamaa