Mwl.Nyerere alimkuta Mfalme wa kichaga(mangi) akitafuta uhuru wa Kilimanjaro pekee?

Mwl.Nyerere alimkuta Mfalme wa kichaga(mangi) akitafuta uhuru wa Kilimanjaro pekee?

munisy2013

Member
Joined
Apr 19, 2013
Posts
9
Reaction score
2
Wana JF salam,kunakuwaga na tetesi Mwl JK Nyerere alipofika UK kutafuta kupewa uhuru wa Tanganyika alimkuta mmoja wa wafalme (mangi)wa kichaga nae akitafuta uhuru ila yeye alitaka wa Kilimanjaro peke yake,ya kweli?
 
Hiyo ni kweli. Na Nyerere alimwambia nimekukubali Mangi na hakika Kilimanjaro itakuwa ya kwanza kukombolewa kisiasa na kifikra..!
 
Hiyo ni kweli. Na Nyerere alimwambia nimekukubali Mangi na hakika Kilimanjaro itakuwa ya kwanza kukombolewa kisiasa na kifikra..!

Uhuru wa Tanganyika haukutafutwa UK....ila UNO-USA. Nyerere aliona haja ya kuwa na Tanganyika yote na ku mshauri huyo mangi wa Kilimanjaro aache zoezi la kuutaka Uhuru wa kilmanjaro peke yake.... Sababu yake kwakua alikua mkuu wa makabila ya huko hakuwa na uwezo wa kuyasemea makabila ambayo yeye siyo Mangi wao (au mfalme wao) kuliitajika mikataba kuonyesha unawasemea watu unaowatawala... Nyerere ha kufanya kazi kubwa Kilmanjaro kwani tayari watu waliisha amka

Nyerere akawa na ushauri mpana zaidi kwa kuonyesha legitimacy ya TANU kwa Tanganyika na alihitaji ridhaa za watemi wote Tanganyika akiwemo Mangi .., na wakasafiri pamoja kwenda UNO akiwa pamoja na Mangi na walitoa hotuba UNO wote wawili.

Ukitoa hoja ikamilishe ili tuone unataka kujenga nini.... km ni Ukabila au Udini au vinginevyo
 
so far Nyerere was damn smarter,wao machief walikuwa wakifikiria vijieneo vyao vya size ya kisosi,
akawaimbisha wimbo wa Tanu,akachukua nchi akafutilia mbali huo wendawazimu wao wa kichifu....Aha aha.
Nina babu yangu mtoto wa chifu analaani mpaka leo...
but walikuwa wanafkiria too low.
angalia matatizo ya Uganda na Baganda mpaka leo..full collusion since oboe till now..
Kudos Nyerere,uliona mbali sana...
 
Wana JF salam,kunakuwaga na tetesi Mwl JK Nyerere alipofika UK kutafuta kupewa uhuru wa Tanganyika alimkuta mmoja wa wafalme (mangi)wa kichaga nae akitafuta uhuru ila yeye alitaka wa Kilimanjaro peke yake,ya kweli?

Si vbaya kwa sababu tangu wakoloni wanaingia na kuanzisha tawala zao kulikuwa na vugu vugu la kuwapinga kutoka kwa Machifu na Viongozi wa makabila km Mkwa- Wahehe, Songea - Wangoni, Mirambo - Wanyamwezi. Baada ya Mwal. Nyerere kuanza harakati akaona na vizuri wote waunganishwe na kudai uhuru kwa pamoja kama nchi kuliko kabila moja moja. Hata Mwal. Nyerere na Kwame Nkrumah walikuwa na mwono wa kuwa na Afrika moja, lakini kila mmoja alipigania uhuru wa chi yake kwanza. Kwa hiyo huyo Mangi anapaswa kupongezwa kwa kukubali maoni ya Mwal. Nyerere, hakuna sehemu katika historia inayoonyesha kuwa huyo Mangi alikataa kumwuunga mkono. Ni swala la kupongezwa badala ya kubezwa, vinginevyo, angeweza kukataa na kuendelea na kudai uhuru wa Kilimanjaro pekee kitu ambacho kilikuwa kinapendwa na wakoloni katika mfumo wa "Divide and rule".
 
Si vbaya kwa sababu tangu wakoloni wanaingia na kuanzisha tawala zao kulikuwa na vugu vugu la kuwapinga kutoka kwa Machifu na Viongozi wa makabila km Mkwa- Wahehe, Songea - Wangoni, Mirambo - Wanyamwezi. Baada ya Mwal. Nyerere kuanza harakati akaona na vizuri wote waunganishwe na kudai uhuru kwa pamoja kama nchi kuliko kabila moja moja. Hata Mwal. Nyerere na Kwame Nkrumah walikuwa na mwono wa kuwa na Afrika moja, lakini kila mmoja alipigania uhuru wa chi yake kwanza. Kwa hiyo huyo Mangi anapaswa kupongezwa kwa kukubali maoni ya Mwal. Nyerere, hakuna sehemu katika historia inayoonyesha kuwa huyo Mangi alikataa kumwuunga mkono. Ni swala la kupongezwa badala ya kubezwa, vinginevyo, angeweza kukataa na kuendelea na kudai uhuru wa Kilimanjaro pekee kitu ambacho kilikuwa kinapendwa na wakoloni katika mfumo wa "Divide and rule".

Kuna baadhi ya watu walimpinga Nyerere sana tu kwa kitendo chake cha kuwaunganisha watu wa Kilimamnjaro in what was that time called Tanganyika, eti kisa, wao walikuwa na elimu zaidi, na pia kulikuwa kuna hofu kwamba watachukua aridhi yao.

Ukiangalia situation iliyopo leo, it is undisputable that this is an ongoing crisis, mwisho wake utakuwaje, only God knows and may be some few smart fox out there. Nyerere angekuwepo angekuwa in a much better position to explain it.
 
Kama lengo lako lilikuwa kujua tu bila shaka umejibiwa, lakini kama una hoja zaidi ya hayo tunakusubiri
 
Mwana JF

Inaonekana kwamba unadhani ni Mwalimu Nyerere mwenyewe aliyepigania uhuru wa Tanganyika. Hii si kweli:

Wale WaTanganyika walioanzisha T.A.A. na baadaye wakamkaribisha Nyerere aliyekuwa akifundisha Sekondari ya Pugu ndio walianzisha siasa dhidi ya mkoloni hapa nchini. Pia ingefaa utambue kwamba hata Vita vya MajiMaji dhidi ya Wajermani vilianzisha mwamko kwamba sisi WaTanganyika tulikuwa taifa "in embriyo".

Ni kweli Thomas Marealle, Paramount Chief of Wachagga, alienda kuhutubia UNO Assembley wakati huo Nyerere akienda. Kabla ya hapo Jafet Kirillo wa Meru alihutubia Kamati ya UNO pia kuhusu tatizo la ardhi kwa kabila lake.

Juhudi za Nyerere ziliungwa mkono na watemi au wamangi wengi Tanganyika. Hata ukisoma orodha ya Watanganyika waliokuwa wameteuliwa kuingia Legco ya mwanzo utaona majina ya Watemi/Wamangi wengi: Nitaje Chief Kidaha Makwaiya wa Shinyanga, Usukuma, Chief Humbi Ziota, Chief Abdallah Fundikira, Chief Patrick Kunambi wa Morogoro na Chief Adam Sapi Mkwawa aliyeng'ara na kuwa Spika wetu wa Uhuru.

Niseme pia kwamba kuna aina ya upotoshaji kutamka eti Chief wa Wachagga alikuwa UNO kutetea uhuru wa Kilimanjaro peke yake. Kama alisisitiza tatizo la ardhi iliyokuwa imepokonywa na masetla wa Kizingu katika eneo lake, labda na haja ya kuhimiza elimu kwa watoto, hayo ndiyo yalikuwa ni mambo muhimu yaliyokuwa yanazungumzwa katika Chagga Council aliyokuwa anaiongoza na iliyomlipia nauli kwenda UNO.

Nisisitize hapa pia kwamba Mwalimu Nyerere wakati huo alikuwa anahitaji ushirikiano wa machifu ili kuendeleza madai ya uhuru, licha ya kwamba wengi wa hawa machifu hawakuwa wanaamini kwamba uhuru upiganiwe uje mapema kama Nyerere alivyotaka. Hata hivyo, kule Uchagani kulikuwa na machifu progressive kama John Maruma, aliyekuwa Makerere College pamoja na Nyerere na wengine kama Petro Itosi Marealle na Abdiel Shangali. Inavyofahamika, baadhi ya hawa machifu walikuja kushiriki katika Serikali ya Nyerere katika kuongoza taasisi za umma kama Civil Service Commision, Transport Licensing Board etc baada ya Serikali kufuta uchifu wa jadi.
 
Watu wengi watajaribu kupotosha ukweli kuhusu J. K. Nyerere lakini mwisho wa siku wanagwaya. Endeleeni na hawa waporaji wasiokuwa na hadhi ya kuwa viongozi, ambao bila Nyerere wasingeweza hata kwenda kusoma huko wanakosema wamesoma lakini hawaelewi. Kabla hujafa hujaumbika.
 
Back
Top Bottom