Mwongozo wa kununua gari iliyotumika

Ozzie

JF-Expert Member
Joined
Oct 9, 2007
Posts
3,217
Reaction score
1,261
Unapotafuta kununua gari iliyotumika (used/second), uamuzi wa kujua gari ipi itakufaa utategemea mahitaji, bajeti, na mapenzi yako binafsi. Haya ni baadhi ya maswali yanayoweza kukuongoza kufikia maamuzi sahihi:


  1. Je, itakuwa ni gari pekee au una gari nyingine ambalo litakuwa na matumizi madogo au sawa au litatumika mara kwa mara?
  2. Je, utakuwa ukitumia gari kwa safari fupi au ndefu za mara kwa mara?
  3. Je, una wazo lolote kuhusu umri wa gari unalolihitaji au umbalo ambao lishakwisha tembea?
  4. Je, una upendeleo wowote wa kampuni ya gari (mfano Toyota, BMW, Land Rover n.k.) au aina ya gari (mfano Prado, Range Rover n.k) au rangi?
  5. Je, unategemea kubeba watu wangapi kwa wastani?
  6. Je, wataka nafasi ya ziada nyuma ya gari ili kubeba vitu vya ziada?
  7. Je, wapendelea gari zilizopanda juu?
  8. Je, vitu gani vya gari vina umuhimu zaidi kwako vilivyotajwa hapo chini?

  • Usalama
  • Matumizi ha mafuta
  • Ukubwa wa gari
  • Idadi ya milango ya gari
  • Gharama za kuliendesha gari ikiwa pamoja na upatikanaji spare na mafundi
  • Gharama za bima
  • Four wheel
  • Gharama za kununua gari
  • Uzoefu wa kuliendesha
  • Nafasi ya ndani
  • Nguvu ya gari
  • Thamani yake ukitaka kulituma tena (Resell value)
  • Vikorombwezo uvitakavyo kwenye gari
Je, mmiliki wa sasa ni mnunuzi wa kwanza wa gari lingali jipya?

Je, una bajeti ambayo haiwezi kuongezaka?

Maswali kama hayo yanaweza yakakupa pa kuanzia.
 
mwongozo wako umekaa vyema kiuchambuzi hasa kumfaa mtu kiuchumi.......niliandika hapa gari(used, but in good condition) lahitajika, bado demand ni open..
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…