My 2024 in a nutshell

My 2024 in a nutshell

Dizasta Vina

Member
Joined
Jul 15, 2021
Posts
16
Reaction score
53
Mwaka 2024 umetupisha, Nilipitia vitabu kadhaa, filamu kadhaa, albums kadhaa za muziki kwa mwaka huo wote. Nimeandaa list yenye baadhi ya nilivyovipenda zaidi.

VITABU​

Mwaka huu nilisoma vitabu vitatu na hii ndio review yangu kwa ufupi kwa kila kimoja.

1. Ujamaa - Essay on Socialism - The late Julius K. Nyerere


Kitabu kilichapichwa kwa mara ya kwanza mwaka 1961, na kufanyiwa marejeo mara kadhaa na baadaye kutafsiriwa kwa lugha ya kiingereza mwaka 1968. Nilikisoma kwa mara ya kwanza mwaka 2013 lakini nikawiwa kurudia sasa nikiamini kuwa na uwezo wa kuelewa maudhui yake kwa mapana yake. Kwenye nakala hii mwandishi anajadili maono ya hayati Baba wa taifa Julius Kambarage Nyerere kuhusu wazo lake la kuwepo kwa aina maalumu ya ujamaa inayoendana kwa asilimia mia moja na tamaduni, mira na desturi, aina ya itikadi, kiwango cha uelimikaji na mtindo wa maisha wa nchi za kiafirka (Specifically Tanzania). Wazo la aina hii ya ujamaa lilitumika kama sera kuu ya chama cha siasa cha TANU ambacho Mwalimu alikuwa ni mwenyekiti wake. Mwandishi alielezea mafanikio na changamoto ya wazo hili hasa kwenye practicability and implimitations. Nakala hii ilibaki kumbukumbu ya juhudi za mwanzo za kumkomboa mwananchi masikini baada ya Ukoloni. Hili andiko lilisanifisha kanuni muhimu zilizosimamia haki na usawa kama zilivyojadiliwa kwenye azimio la Arusha. Nukuu yangu pendwa kutoka kwenye nakala hii ni ile iliyomnukuu mwalimu kuhusu umuhimu wa kufanya kazi kwa bidii kwa ustawi wa familia zetu, akisema "‘Mgeni siku mbili; siku ya tatu mpe jembe’

2. The moral Lanscape - How science can determine human values - Sam Harris

Binadamu wa karne ya 21 wamekuwa kama kitu kimoja kwa sababu ya kukua kwa teknolojia hasa kwenye eneo la mawasiliano na usafirishaji. kukua huku kumefanya dunia kuwa ndogo. Binadamu wanajijamiisha kwa karibu na kwa haraka zaidi bila kujali maeneo waliopo. Hii imekuza umuhimu wa mazungumzo kuhusu falsafa ya maadili. Mwandishi wa The Moral Landscape, Kitabu kilichochapishwa mwaka 2010, Sam Harris anajadili wazo la kuhusianisha maadili na ustawi wa maisha ya binadamu (Well-being) akisema Mijadala ya maadili haitakuwa na maana kama haitahusisha ustawi wa maisha ya binadamu na wanyama. Pia alijadili kwa kiasi gani sayansi itaweza kutupa kweli ya nini maana ya ustawi hasa kwenye eneo la afya ya akili, mwili na hisia za binadamu. Pia alijadili tamaduni na imani mbalimbali zinavyoweza kuhatarisha afya ya mwili, akili na hisia, lakini pia afya ya uchumi wa binadamu. Nukuu yangu pendwa kutoka kwenye kitabu hiki ni "Wanawake na wanaume walio kwenye hukumu za kunyongwa, wapo pale kwa sababu ya mchanganyiko wa malezi mabaya, mawazo na itikadi mbaya, imani mbaya, vinasaba mbaya au bahati mbaya"

3. Who we wrestle with God - Jordan Peterson

Kitabu hiki kilichapishwa November 2024, Ndio kilikuwa kitabu cha mwisho kusoma mwaka huu. Mwandishi anajadili hadithi za mwanzo kabisa za kifasihi na umuhimu wake kwenye maisha ya sasa. Mwandishi anaamini kuwa fasihi za zamani ni muhimu kwa sababu zinatupa picha ya mtindo wa kufikiri wa jamii za kale (their thinking process). Mwandishi pia anajadili dhana ya ukaidi, sadaka, mateso na ushindi kwa kutumia hadithi mbalimbali za kibiblia. Jordan anachagua Biblia kuelezea subject matters zake akiamini ni kitabu stahiki zaidi kiushawishi, kiumri na kiuhalisia (authenticity). Moja ya subject matter alizojadili mwandishi ni IMANI na kujitoa SADAKA (Faith and sacrifice). Anasema dunia na mapana ni kubwa sana kiasi hatuwezi kuimaliza kuielewa hivyo kwenye maisha mafupi ya binadamu huwa tunachagua vile tunaavyoona ni muhimu. Na hapo ndio Imani na sadaka vinapokuja kwani kuchagua ni kuamini kuwa upo sawa na machaguo yako na unatoa sadaka vingine vyote ili kufuata unachoona ni sahihi (cost of choices/opportunity). Mfano wa hadithi alizotumia kujadili maudhui ni ile hadithi ya Yona aliyeikimbia sauti ya Mungu iliyomtuma kwenda Nineveh kueneza habari njema, Yona alikaidi na mwishowe kumezwa na samaki. Mwandishi alihusisha hii hadithi na athari za kukimbia majukumu kwa nafasi uliyopewa. Nukuu yangu pendwa kwenye kitabu hiki ni "kanuni mbaya zikienziwa, wafalme wabaya wakisimamishwa na maadili mabaya yakiwekwa na watu, ni watu wenyewe ndio wataangamia"

FILAMU​

Nilipata wasaa wa kuangalia filamu kadhaa mwaka 2024 na hizi ni 5 zilizonivutia zaidi.
1. 12 angry men ya mwaka 1957

Filamu inahusu baraza la waamuzi 12 waliopewa jukumu na mamlaka ya kuamua kesi ya kijana aliyetuhumiwa kumuua mzazi wake. Kesi iliyoonekana ni ya dakika kadhaa tu kwa sababu ya nguvu ya ushahidi uliowekwa ila inageuka kuwa shughuli ya kichunguzi. Waamuzi 11 waliamini kuwa mtuhumiwa ni mkosefu na anastahili adhabu wakati mmoja akiwa na shaka na aina ya ushahidi ulioletwa, hivyo akachukua jukumu kuwashawishi waamuzi wenzake kujadili upya ushahidi ili kuondoa shaka. Filamu ya seti moja ila ilikuwa na uwezo wa kubakisha shauku muda wote kwa sababu ya ubora wa mazungumzo na story progression. Moja ya nukuu niliyoipenda kwenye Filamu hii ni "Kama unataka kupiga kura kuwa fulani ana hatia, sema kwa sababu una uhakika ana hatia na sio kwa sababu umechoka kusikiliza shauri". Mtoa nukuu alikuwa anajaribu kuwaambia waamuzi wengine kuwa wasitoe maamuzi wa sababu wamechoka na wanataka kwenda nyumbani

2. Schindller's list -1993

Filamu ya wasifu wa kweli (Autobiography) inayomuhusu Oskar Schindler, Mfanyabiashara mwenye tamaa ya pesa aliyeingiwa na ubinadamu kiasi kugeuza kiwanda chake kuwa kimbilio la wayahudi waliothiriwa na serikali ya ki-nazi ya Ujerumani. Filamu hii iliandaliwa kuenzi mchango wa Oskar kwenye mapambano dhidi ya ukatili wa serikali ile chini ya Adolf Hitler. Moja ya nukuu muhimu niliyoipenda kwenye Filamu hii ni "Nguvu ni pale ukiwa na kila sababu ya kuua alafu hauui" akijadili umuhimu wa kusamehe na moja ya wafanyakazi wa serikali ya kibazazi ya ujerumani.

3. Enemy - 2013

Filamu ya kisaikolojia inayomuhusu mhadhiri wa chuo kikuu anayemuona mtu anayefanana naye kwa asilimia 100 kwa mara ya kwanza baada ya kuambiwa na rafiki yake kuwa wamefanana. Anaenda kuangalia filamu zake baada ya kugundua ni mwigizaji. Kiu ya kumchunguza inaishia kumuweka kwenye njiapanda inayozaa matatizo makubwa. Mhadhiri huyu analea mazoea yake ya kuchunguza familia ya mtu huyu na mwishowe kuingia matatani. Filamu inayojadili umuhimu wa kurekebisha mazoea mabaya kabla hayajawa tabia. Mazoea kwenye filamu yanawakilishwa na buibui mdogo anayeonyeshwa mwanzo wa filamu kisha kuwa mkubwa mwisho wa filamu.

4. The Assasionation of JESSE JAMES by the Coward ROBERT FORD - 2007

Mja mwoga Robert Ford anategemea kulakiwa kishujaa na jamii yake baada ya kumuua jambazi anayeogopwa kwenye mji wake. Kiu ya umaarufu na heshima inamfanya kubadili jina kisha kuandika kitabu kusheherekea mauaji yake mwenyewe lakini bado jambazi Jesse anaimbwa kama shujaa huku yeye akiwa hatambuliki kabisa. Hasira inampanda baada ya filamu kutengenezwa kumuenzi Jesse. Robert anajaribu kuishi na uhalisia kuwa watu hawamwoni kama shujaa bila mafanikio, Kiu yake ya kuheshimiwa inarudi na mwishowe inamwingiza kwenye kifo.

5. Cosmos: A Spacetime Odyssey, Season 1
Msimu wa kwanza wa mfululizo wa sukununu ya binadamu kuhusu ulimwengu na elimu ya anga. Chaneli ya National Geographic wanaungana na Mkufunzi wa masuala ya astrofizikia Neil de Grease Tyson kubadili kitabu kuwa onyesho la televisheni.

ALBUMS​

Nilisikiza album kadhaa kwa minajiri ya burudani na elimu na hizi ndio zilinivutia zaidi.

1. The auditorium Vol 1 by Common & Pete Rock
2. Knock Madness by Marcus Hopsin
3. Mapinduzi halisi by Professor Jay
4. Extiction level Event 1 by Busta Rhymes
5. Extiction level Event 2 by Busta Rhymes
6. Mhadhiri by Maalim Nash
7. Mitaa flani by Songa
8. In my room by Jacob Collier
9. Dawn by Yebba

Soma zaidi dizastavina.com

Dzstvn%202024%20Recap.png
 
Thanks mkuu.

Not necessarily this year.

Katika vitabu vyako ninesoma 1 na 2.

Movies nimeona 1, 2 na 5

Albums 2,3,4,5,6,7.

Shukurani kwa list.

12 Angry Men is one of my top movies.

Nitatafuta movies na albamu ambazo sojapitia.

Hicho kitabu cha Jordan Peterson nafikiri ninacho lakini sijakisoma.
 
Nimesikiliza summary ya hivyo vitu vyote kupitia AFF
 
Back
Top Bottom