Pre GE2025 Mzazi/Mlezi, Ungependa Binti yako awe Mwanasiasa?

Pre GE2025 Mzazi/Mlezi, Ungependa Binti yako awe Mwanasiasa?

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)

Lady Whistledown

JF-Expert Member
Joined
Aug 2, 2021
Posts
1,147
Reaction score
2,008
“Wazazi na walezi, je, mnaona umuhimu wa mabinti wenu kujihusisha na siasa?

Je, mko tayari kuwaunga mkono katika safari hiyo ya uongozi na mabadiliko?

Tushirikiane mawazo!
 
“Wazazi na walezi, je, mnaona umuhimu wa mabinti wenu kujihusisha na siasa?

Je, mko tayari kuwaunga mkono katika safari hiyo ya uongozi na mabadiliko?

Tushirikiane mawazo!
Mimi kama mzazi sitatamani binti yangu awe mwanasiasa, sitatamani kabisa, japo kuna wengine wanajikuta wameingia kwenye siasa kwa sababu ya promotion kutoka kwa wakuu, kwa mfano ukiteuliwa kuwa mkuu wa wilaya automatically unajikuta umekuwa mwanasiasa
 
“Wazazi na walezi, je, mnaona umuhimu wa mabinti wenu kujihusisha na siasa?

Je, mko tayari kuwaunga mkono katika safari hiyo ya uongozi na mabadiliko?

Tushirikiane mawazo!
Mimi mke wa mtu siwezi kumruhusu awe kiongozi.

Msimamo wangu ni tofauti kidogo na watu wengine na naamini Kwa mitazamo ya watu naweza kuonekana ni mtu wa ajabu lakini katika kuhakikisha thamani ya mwanamke inakuwa juu zaidi kulingana na Mila na desturi zetu za kiafrika Bado naamini mwanamke hawezi kusimama kuongoza watu(wanaume).

Ebu tuanze kuchambua kulingana na Familia, koo, jamii, na Dini zetu.

Kwenye familia zetu Bado tunaona baba ndie kiongozi wa familia.

Kwenye koo zetu Bado tunaona viongozi wa ukoo ni mwanaume na hata viongozi wa matambiko Bado ni wanaume.

Kwenye jamii zetu hasa tukihusisha masuala ya ndoa Bado tunaona wanaume ndo wanaooa wanawake na mwanamke ambaye ataolewa jina lake linabadilika na huitwa na kutambulika Kwa jina la mume wake na watoto atakao wazaa pia wataitwa Kwa jina la mume wake.

Kwenye Dini zetu hasa Dini ya kiislamu na kikristo Bado viongozi wa Ibada ni wanaume.

HITIMISHO: Sina lengo la kuvunja Nia na nguvu ya mwanamke Bali Nia na Lengo ni kuwaambia wanawake kwamba uongozi uanzie nyumbani katika ngazi ya mke na mume kama wanazani ni jambo halali na ni haki kwao.
 
Labda ajiunge na ccm maana ndio wanambeleko ya vyombo vya dola. Lakini akijiunga na upinzani ajiandae kutekwa ama kuuwawa kama atakuwa na ushawishi wa kisiasa.
 
Labda ajiunge na ccm maana ndio wanambeleko ya vyombo vya dola. Lakini akijiunga na upinzani ajiandae kutekwa ama kuuwawa kama atakuwa na ushawishi wa kisiasa.
Nakubakwa
 
Hakuna umuhimu wowote ni kujiletea matatizo tu
 
Labda ajiunge na ccm maana ndio wanambeleko ya vyombo vya dola. Lakini akijiunga na upinzani ajiandae kutekwa ama kuuwawa kama atakuwa na ushawishi wa kisiasa.
Siasa Ina ngono sana, STAKI mwanangu wa kike awe...Kuna rushwa ya ngono sana
 
Yaani unaitwa na wakubwa wa chama kwa mfano mwenyekiti wa ukanda flan uende hotel flan..

Unashangaa unakuta chumba kizuri unaambiwa "ukiyeitiwa ana kikao msubiri..."

Few moment later "........." ●$}~♧₩📥😭♤•♤•♡\$|€374747¿


Chakula kinaliwa usiku kucha
 
“Wazazi na walezi, je, mnaona umuhimu wa mabinti wenu kujihusisha na siasa?

Je, mko tayari kuwaunga mkono katika safari hiyo ya uongozi na mabadiliko?

Tushirikiane mawazo!
Kwangu mimi ni mwiko,mwanangu au ndugu atakaye jiingiza huko namkana na asinijue.
 
Back
Top Bottom