kavulata
JF-Expert Member
- Aug 2, 2012
- 13,778
- 14,214
Michezo ni furaha na furaha ni kushinda na kushinda ni mipango na sayansi ya michezo na mipango na sayansi ya michezo ni gharama kubwa ambayo mzee Akilimali hamudu hata kununulia wachezaji wa Yanga japo maji ya kunywa tu timu inapokuwa mazoezini licha ya kuwa kwenye mechi uwanjani. Zama za mpira wa ridhaa na kutegemea uchawi ili kupata ushindi zimekwisha. Timu ni Mashabiki na mashabiki wa Yanga wanataka ushindi ili wafurahi bila ya kujali timu inamilikiwa na nani
Mzee Akilimali nadhani hofu yake kuu ni kukosa kifungua kinywa kama timu ya Yanga ikiendeshwa bila kuhakikishiwa upatikanaji wa futali yake. Yuko tayari kutembeza bakuli kwa watu ili apate fedha za kununulia maji wachezaji na yeye kuambulia chochote.
Kote duniani club huwa zinauzwa ili kupata mafanikio ya kiuchumi, ushindi na furaha kwa wanachama na mashabiki wao, iweje Akilimali ang'ang'anie kuwaudhi mashabiki wanaotaka furaha kupitia Yanga?
Yanga ina mashabiki wengi sana, na sauti yao ni sauti ya Mungu, dua zao ni uchawi tosha.
Kama kuna tajiri bila kujali ni Manji au mwingine yule mwenye uwezo wa kutupatia furaha kupitia Yanga ni vema akapewa nafasi.
Mzee Akilimali nadhani hofu yake kuu ni kukosa kifungua kinywa kama timu ya Yanga ikiendeshwa bila kuhakikishiwa upatikanaji wa futali yake. Yuko tayari kutembeza bakuli kwa watu ili apate fedha za kununulia maji wachezaji na yeye kuambulia chochote.
Kote duniani club huwa zinauzwa ili kupata mafanikio ya kiuchumi, ushindi na furaha kwa wanachama na mashabiki wao, iweje Akilimali ang'ang'anie kuwaudhi mashabiki wanaotaka furaha kupitia Yanga?
Yanga ina mashabiki wengi sana, na sauti yao ni sauti ya Mungu, dua zao ni uchawi tosha.
Kama kuna tajiri bila kujali ni Manji au mwingine yule mwenye uwezo wa kutupatia furaha kupitia Yanga ni vema akapewa nafasi.