Mzee Akilimali anahurumia tumbo lake tu

Yaani kama Yanga wanataka wapoteane mpaka kushuka daraja msimu huu ,basi wamchezee huyu mzee,hawa wazee ndo wanaojua Yanga Fc imelalia wapi.
Huyu hana lolote aliwahi sema atahakikisha anaifunga Simba mara tano mfululizo matokeo yake Okwi akatupiga, ni wa kupuuzwa.
 
sawa lakini kwenye hili akina mzee Akilimali hawajitokezi kama whistle blowers bali wanaopenda kubakiza status quo kwa hofu kuwa wao binafsi watapata nini kama mabadiliko yoyote kwe vilabu yatatokea. kwani itatokea nini kama Manji atabanwa kujenga uwanja kulipa makocha na wachezaji kuisafirisha timu klabu mwenyewe kwa kipindi chote cha miaka 10? ni nani atapata hasara kama Manji akipata 75% pamoja na kuihudumia klab?
 
wanataka status quo kwenye vilabu kwa faida zao lakini sio whistle blowers. kama Simba na Yanga zingekuwa zinafanya vizuri kiuchumi kusingekuwa na sababu za kuwasikiliza akina Manji na huenda tungetafuta wanunuzi wa vilabu vyetu kwa kutangaza tender ili kuruhusu ushindani lakini kwa Yanga na simba zilivyo sasa ni first in first out maana kocha na wachezaji wanahitaji fedha ambazo akina nanihii hawanazo. sioni ubaya mtu akichukua 51% pamoja na kuigharimia club kulivyo hivi sasa akina nanihii wanamiliki 100% lakini hawawezi hata kununua mipira ya mazoezi
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…