Mzee Juma katueleza kisa alivyotapeliwa na wanawake huko Facebook

Mzee Juma katueleza kisa alivyotapeliwa na wanawake huko Facebook

mockers

JF-Expert Member
Joined
Nov 19, 2013
Posts
12,843
Reaction score
35,442
Hapa hua tunakutana kwenye tangawizi na kahawa

Mzee juma kafika na kanzu yake swafi na baraghashia yake kama kawaida, Mzee juma siku hizi ana simu ya kupangusa vidole hivo anakua busy kwenye simu , sio kama zamani alipokua anatumia kitochi,

Hussein anamuuliza kiutani mzee J naona unaperuzi mtandaoni, Mzee Juma akastuka ikabidi awe makini na kundi letu pembeni,

Hapa Pana lopolopo mmoja anaitwa Dulla ndio kayazua kumbe Dulla anajua story nzima ya mzee juma kupigwa kama elfu 50 za vocha huko Facebook,

Dulla anasanua michongo yote anaanza hivi mzee Dulla wale watu wako wanaokuomba vocha za Tigo tena utume Tigopesa ili mkachat WhatsApp maana kule hawana bando bado unaendelea nao?

Watu tunastuka akilini tunajua mzee hapo hua anapigwa, Kaeleza kua alipata marafiki huko mabinti wadogowadogo akaambiwa atume vocha wakachat huko mwingine,

Wakihamia huko anaambiwa atume elfu kumi waongee video call, naye anatumia, Hapa naona kuanzia kesho mzee Juma hatokuja kijiweni hadi hali ipoe kidogo maana kila mmoja anamcheka.

Kupitia kisa cha mzee juma nimekumbuka baadhi ya mbinu za utapeli , mfano umpeleke hela zako zote zikalale kwa mganga na kesho unakuta hayupo na pesa kaondoka nayo. Kupigiwa simu za kuhusu tenda za ujenzi, uchimbaji wa visima, madawa ya kilimo na mifugo wote huo utapeli.
 
Kupigiwa simu kua kuna pesa imeingia kwako hivo uirudishe hapo hutakiwi kufuata maelekezo yoyote simple kama wamekosea muamala wanatakiwa kuusigisha wao hapo kuna utapeli
 
Utapeli wa wauza madawa ya asili wale wanaotembea na spika na vitabu na dawa kwenye chupa , wanawakusanya wanaanza na vitisho then mnapewa vijitabu uchwara ule ni utapeli
 
Wauzaji wa bidhaa mbalimbali kwenye mabasi safarini wale ni matapeli hakuna promotion pale unanunua bidhaa overprice
 
Ukiona pesa inaangushwa mbele yako halafu unaambiwa mkagawane akiwa kaokota mwingine hapo stuka ni matapeli
 
Kuuziwa kitu feki baada ya kuoneshwa kitu halisi yaani inatakiwa ukae macho hapo kuna bidhaa kama simu , unaweza kupewa sabuni ule hua ni utapeli
 
Utapeli kwenye ununuzi wa viwanja , inabidi ukae makini ukikneshwa kiwanja usiishie ofisi ya mtaa tu , usilipe pesa haraka , tafuta majirani watatu au wanne wenyeji kwa nyakati tofauti upate historia ya eneo ndio ufanye maamuzi yako
 
Utapeli wa kuambiwa mtu atalima au atafuga wewe ukiwa nyumbani halafu utapokea pesa tu hapo ni uongo usiweke pesa yako huko utapigwa, Mr kuku iwe mfano , kilimo cha vanilla na maguruwe zile ni scam kama scam nyingine
 
Hapa hua tunakutana kwenye tangawizi na kahawa
Mzee juma kafika na kanzu yake swafi na baraghashia yake kama kawaida,
Mzee juma siku hizi ana simu ya kupangusa vidole hivo anakua busy kwenye simu , sio kama zamani alipokua anatumia kitochi,
Hussein anamuuliza kiutani mzee J naona unaperuzi mtandaoni,
Mzee juma akastuka ikabidi awe makini na kundi letu pembeni,
Hapa Pana lopolopo mmoja anaitwa dulla ndio kayazua kumbe dulla anajua story nzima ya mzee juma kupigwa kama elfu 50 za vocha huko Facebook,
Dulla anasanua michongo yote anaanza hivi mzee dulla wale watu wako wanaokuomba vocha za Togo tena utume tigopesa ili mkachat WhatsApp maana kule hawana bando bado unaendelea nao?
Watu tunastuka akilini tunajua mzee hapo hua anapigwa,
Kaeleza kua alipata marafiki huko mabinti wadogowadogo akaambiwa atume vocha wakachat huko mwingine,
Wakihamia huko anaambiwa atume elfu kumi waongee video call, naye anatumia,
Hapa naona kuanzia kesho mzee juma hatokuja kijiweni hadi hali ipoe kidogo maana kila mmoja anamcheka ,
Kwa majina hayo mimi sichangii lolote maana utaambiwa umewakashifu watu
 
Baba mkwe akinisikiliza kwa umakini nikimsomea hiki kisa ili kesho na kesho kutwa yasimkute ya mzee Juma
FB_IMG_1729026334279.jpg
 
Back
Top Bottom