TANZIA Mzee Kavana (alishiriki Maasi ya 1964) afariki dunia!

TANZIA Mzee Kavana (alishiriki Maasi ya 1964) afariki dunia!

Lole Gwakisa

JF-Expert Member
Joined
Nov 5, 2008
Posts
4,768
Reaction score
2,361
1723302649109.png


1723292715899.png

Mzee Kavana, aliyekuwa Captain Kavana mwaka 1964 na aliyechagulia na askari wa Tanganyika Rifles walioasi ili awe kiongozi wao badala ya wazungu, amefariki jana 9/8/2024.

Captain Kavana wakati huo alikuwa hana hili wala lile huku askari waasi wakishinikiza kuwa kwa vile tumepata uhuru, lazima tuongozwe na muafrika, wakati huo kuna wimbi la Africanisation ya sehemu zote za ungozi nchini.

Hili lilimletea matatizo mzee Kavana maana hakuhusika na maasi wala kuwepo kuyapanga , lakini askari wa chini ndiyo walipenda waongozwe na askari Ofisa mzalendo badala ya wazungu.

Mzee Kavana ameishi kwa utulivu na amani nyumbani kwake Chang'ombe miaka yote.

RIP Mzee Kavana
NB
Picha kwa msaada wa wachagiaji.
Na kunaradhi, cheo wakati wa maasai kwa mzee Kavana alikuwa Luteni.
 
Mzee Kavana, aliyekuwa Captain Kavana mwaka 1964 na aliyechagulia na askari wa Tanganyika Rifles walioasi ili awe kiongozi wao badala ya wazungu, amefariki jana 9/8/2024.

Captain Kavana wakati huo alikuwa hana hili wala lile huku askari waasi wakishinikiza kuwa kwa vile tumepata uhuru, lazima tuongozwe na muafrika, wakati huo kuna wimbi la Africanisation ya sehemu zote za ungozi nchini.

Hili lilimletea matatizo mzee Kavana maana hakuhusika na maasi wala kuwepo kuyapanga , lakini askari wa chini ndiyo walipenda waongozwe na askari Ofisa mzalendo badala ya wazungu.

Mzee Kavana ameishi kwa utulivu na amani nyumbani kwake Chang'ombe miaka yote.

RIP Mzee Kavana
Umeeleza alikuwa hana hili na lile na walioshiriki ni wengine.Mbona kichwa cha habari kinamjumlisha?
 
Ukisikia nongwa ndio hiyo iliyomtokea huyu Captain enzi zake. Mtu mmoja asiyekupenda anajua wazi tukio litashindikana ivyo anakupendekeza kwa wasiokuzingatia kisha wanakuchagua kuwaongoza kwenye usiloshiriki nao.

Yanatokea yakutokea, mtesi anafurahia.

Namuelewa sana yule mwalimu aliegomea ule uteuzi.
 
Ukisikia nongwa ndio hiyo iliyomtokea huyu Captain enzi zake. Mtu mmoja asiyekupenda anajua wazi tukio litashindikana ivyo anakupendekeza kwa wasiokuzingatia kisha wanakuchagua kuwaongoza kwenye usiloshiriki nao.

Yanatokea yakutokea, mtesi anafurahia.

Namuelewa sana yule mwalimu aliegomea ule uteuzi.
Kama kupewa uongozi wa Hamas tu unachaguliwa huku wasiokupenda wanaenda kuchekea chooni kwamba huyu muda wowote kivumbi kinamtokea
 
Mzee Kavana, aliyekuwa Captain Kavana mwaka 1964 na aliyechagulia na askari wa Tanganyika Rifles walioasi ili awe kiongozi wao badala ya wazungu, amefariki jana 9/8/2024.

Captain Kavana wakati huo alikuwa hana hili wala lile huku askari waasi wakishinikiza kuwa kwa vile tumepata uhuru, lazima tuongozwe na muafrika, wakati huo kuna wimbi la Africanisation ya sehemu zote za ungozi nchini.

Hili lilimletea matatizo mzee Kavana maana hakuhusika na maasi wala kuwepo kuyapanga , lakini askari wa chini ndiyo walipenda waongozwe na askari Ofisa mzalendo badala ya wazungu.

Mzee Kavana ameishi kwa utulivu na amani nyumbani kwake Chang'ombe miaka yote.

RIP Mzee Kavana
Labda ni kwa vile marehemu hasemwi vibaya, ila kwa kuweka rekodi sawa nadhani ni sawa kuelezea jambo hili kwa jinsi lilivyokuwa, kwani ni sehemu ya historia ya hii nchi tuliyopo leo na vizazi vyetu.

Kiukweli, kwa namna hadi Luteni Elisha Kavana anapendekezwa kuwa kiongozi badala ya Askari wa Kizungu, tayari wote wasiounga mkono uasi ule walikuwa chini ya Ulinzi, na kubaki waliounga mkono.

Wakati Oscar Kambona amefikishwa kwenye kambi ya Colito, Kavana hakuwa chini ya ulinzi, na alikuwa miongoni mwa waliopiga yowe kumkataa Alex Nyirenda aliyetajwa awali kuwa kiongozi.

Hii ni tofauti na ilivyokuwa kwa Mirisho Sarakikya kwa kambi ya Tabora, ambaye aliteuliwa kuwa kiongozi huku akiwa mahabusu, kwani ilibidi atolewe mahabusu na kupewa taarifa, kisha akatoa amri ya kusitisha uasi.

Lakini, Kavana alitajwa jina lake kwa kupendekezwa huku mwenyewe akiwepo na kuvishwa kofia palepale na kushangiliwa, mbele ya Kambona ambaye wakati huo alikuwa ndiye Waziri wa Ulinzi.

Uamuzi uliompa uongozi Kavana ulifanywa na Kambona kwa shinikizo la Sgt. Ilogi na askari waliokuwako Colito wakati huo, akiwemo Kavana, wakimtisha kumpiga risasi Kambona asipotii matakwa yao.

RIP Mzee Elisha Kavana.

Ova
 
Labda ni kwa vile marehemu hasemwi vibaya, ila kwa kuweka rekodi sawa nadhani ni sawa kuelezea jambo hili kwa jinsi lilivyokuwa, kwani ni sehemu ya historia ya hii nchi tuliyopo leo na vizazi vyetu.

Kiukweli, kwa namna hadi Luteni Elisha Kavana anapendekezwa kuwa kiongozi badala ya Askari wa Kizungu, tayari wote wasiounga mkono uasi ule walikuwa chini ya Ulinzi, na kubaki waliounga mkono.

Wakati Oscar Kambona amefikishwa kwenye kambi ya Colito, Kavana hakuwa chini ya ulinzi, na alikuwa miongoni mwa waliopiga yowe kumkataa Alex Nyirenda aliyetajwa awali kuwa kiongozi.

Hii ni tofauti na ilivyokuwa kwa Mrisho Sarakikya kwa kambi ya Tabora, ambaye aliteuliwa kuwa kiongozi huku akiwa mahabusu, kwani ilibidi atolewe mahabusu na kupewa taarifa, kisha akatoa amri ya kusitisha uasi.

Lakini, Kavana alitajwa jina lake kwa kupendekeza huku mwenyewe akiwepo na kuvishwa kofia palepale na kushangiliwa, mbele ya Kambona ambaye wakati huo alikuwa ndiye Waziri wa Ulinzi.

Uamuzi uliompa uongozi Kavana ulifanywa na Kambona kwa shinikizo la Sgt. Ilogi na askari waliokuwako Colito wakati huo, akiwemo Kavana, wakimtisha kumpiga risasi Kambona asipotii matakwa yao.

RIP Mzee Elisha Kavana.

Ova
Kwa kweli maasi yale yalikuwa ya askari wa vyeo vya chini.
 
..anaitwa Meja. Elisha Kavana.

..kama sijakosea alikuwa Mtanganyika msomi mwenye shahada ya chuo kikuu ktk jeshi la Tanganyika [ Tanganyika Rifles. ]

..Tanganyika Rifles waliasi mwaka 1964, na maasi yaliongozwa na Sajent Hingo Ilogi.

..maasi hayo yalizimwa na Jeshi la Waingereza, na kupelekea Tanganyika Rifles kuvunjwa, na kuundwa TPDF / JWTZ.

..Pia baada ya maasi kuvunjwa, na kikosi cha Waingereza kuondoka, wanajeshi toka Nigeria walikuja Tanganyika kulinda amani.
 
Back
Top Bottom