Pre GE2025 Mzee Kinana, kwanini vijana uliowafundisha siasa hawafuati hatua zako za uwajibikaji? Hongera kwa kujiuzulu!

Pre GE2025 Mzee Kinana, kwanini vijana uliowafundisha siasa hawafuati hatua zako za uwajibikaji? Hongera kwa kujiuzulu!

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)

Rabbon

JF-Expert Member
Joined
Apr 16, 2022
Posts
21,625
Reaction score
33,688
1722276830599.png

Mzee Kinana

Salaam, shalom!!

Ndani ya chama Cha MAPINDUZI CCM, umewafundisha siasa vijana wengi sana, inawezekana wamefaulu machache kati ya mengi uliyowafundisha,

Somo linalohusu uwajibikaji wa pamoja umelifundisha sana tena Kwa vitendo, imekuwa mjenga HOJA mzuri, umejiuzulu mara kadhaa pale ulipoona mapungufu ndani ya chama Ili kuonyesha uwajibikaji wa pamoja.

Vijana ndani ya CCM, Nape, Makamba, Bashe ,Mwigulu, Kigwangala, nk nk somo hili wamegoma kulielewa na hawataki kulisikia!!

Swali: Ulikosea wapi katika mafunzo Yako Mzee Kinana, maana unaondoka bila kurithisha ubora wako Kwa vijana waliopo Hasa katika somo la uwajibikaji, nini kifanyike?

Karibuni 🙏

PIA SOMA
Abdulrahman Kinana, Makamu Mwenyekiti (CCM) Ajiuzulu, Rais Samia Suluhu Aridhia
 
Barua ya kuridhia kujiuzulu tumeiona ila ya kuomba kujiuzulu hatujaoneshwa!
Au hakuandika, aliandikiwa?
 
Barua ya kuridhia kujiuzulu tumeiona ila ya kuomba kujiuzulu hatujaoneshwa!
Au hakuandika, aliandikiwa?
Kwakuwa ni Mzee, umri umeenda,

Tuamini ameonba kupumzika,

Swali linabaki, Pana mwanafunzi yeyote wa Kinana ndani ya chama mwenye capacity angalau nusu yake tu wa kushika kijiti au ndio chama kinaenda maghribi kama jua?
 
Back
Top Bottom