Mzee Lowassa hawezi kusahau kipindi hiki cha Richmond

Mmawia

JF-Expert Member
Joined
Aug 20, 2013
Posts
122,494
Reaction score
96,074
Naamini mzee wetu Lowasa hatokaa asahau mzimu wa Richmond.

Kilikuwa ni kipindi kigumu sana kwa waziri mkuu mstaafu.

Alikutana na bunge lenye meno chini ya wabunge wa upinzani ambao bado walikuwa hawajabinafsishwa na ccm.

Mzee wetu aliongea sana hadi akafikia kutoa machozi kwa uchungu wa kukimbiwa na washirika wenzake kwenye huo mchongo wa upigaji.

Your browser is not able to display this video.

Soma
 
Walasio Upinzani Wala Nini!

Dola ilianza kazi rasmi ya kuwasambaratisha wanamtandao ambao walitaka kuifanya nchi ni ya kwao!bila hivyo Leo Wana mtandao wangeamua uraus was nchi hii watakavyo wao!!

Sio upinzani. Wala ccm ,ni dola katika kuua mtandao wao kwa kuwachonganisha!!!
 
Hivi tuseme ni bunge ndio likikuwa na meno, au bunge liliamua kusimama na mtawala kama ambavyo ile ripoti ya Richmond iliyosomwa na Mwakyembe ilivyosema?

Nakumbuka Dr. Mwakyembe mwenyewe kwa kinywa chake alisema anaogopa nchi kutikisika kwa kutosema yote waliyogundua kwenye ule uchunguzi wao.

Mimi naona bunge liliamua kusimama na mtawala, lakini kama kweli bunge lingekuwa na meno, basi kwanza lingemlazimisha Dr. Mwakyembe aseme yote, pili lingepiga kura ya kutokuwa na imani na mtawala, hapo ndio ningelipongeza bunge.

Sent from my SM-G900H using JamiiForums mobile app
 
Kwahiyo sahivi dola ipo likizo? maana majangili yote yamerudi kwenye system
 
Dadadekii chadema wakanusa harufu ya mshiko wakamkomba kumweka kwenye himaya chadema kwa ufisadi wanatisha!
 
Mkuu naomba maana/tafsiri ya neno "kustaafu".
 
Ila baba rizmoko mhuni sana alivyomkataa swahiba wake macho makavu kabisa.
 
We jamaaa , wazazi wako wanajivunia kukusomesha
 
Kwahiyo sahivi dola ipo likizo? maana majangili yote yamerudi kwenye system
Kwa sasa watatokomezwa wote yaani wote hadi mu asisi wa upigaji!!

Wanakusanya ushahidi TU wa Nini kilijiri awamu ya tano!

Wamewapa comfort zone Kwa muda kabla ya kichinjio kufanya kazi yake!!

"SI WAMEKATAA MAAGIZO YA KULETA KATIBA MPYA ILI WAENDELEZE UPIGAJI WAO NA U MUNGU MTU!!?KOSA KUBWA SANA WAMEFANYA LAZIMA DOLA ITASAFISHA WOOTE WANAOHUSIKA,KWA KUWACHONGANISHA WAO KWA WAO HASA HIZO TEAM NA KAMBI NDANI YA CHAMA CHETU"SUBIRI UONE 2024-2025!!!!
 
Hakuna lolote
 
Siyo kweli kwamba 'eti dola ilihusika', ni uongo tupu.

Ila baba rizmoko mhuni sana alivyomkataa swahiba wake macho makavu kabisa.
Absolutely true!
Wale ni marafiki "waliosalitiana" licha ya kwamba mwanzo wa urafiki wao "hawakukutana barabarani."
"Bwana Yule" aliogopa sana kwamba "Richmond" angemzidi kete na kumpindua kwenye mtanange uliokuwa unafuata, umaarufu wa 'Richmond' ulikuwa unakuwa kwa kasi zaidi na mkubwa zaidi kumzidi 'Bwana Yule'. Yaani ilitokea hali ile iliyokuwapo enzi zile za J.K.Nyerere na Edward Moringe Sokoine, it was the same and similar scenario!
 
Dadadekii chadema wakanusa harufu ya mshiko wakamkomba kumweka kwenye himaya chadema kwa ufisadi wanatisha!
Ccm wakaona cdm wanafaidi sana kuwa na fisadi Lowasa wakaamua kumrudisha ccm kundini
 
Ila baba rizmoko mhuni sana alivyomkataa swahiba wake macho makavu kabisa.
Nasikia ingawa siyo ya kuamini kuwa hata yeye alikuwa chini ya shinikizo kubwa kutoka kwa wazee wa lumumba.
 
Ndio unafiki wa ciciemu

Hakuna uwajibikaji kabisa

Unafiki tu

Ukishaweka haya kwa mualifu au mkosefu na wewe unahesibaka katika uovu, kwa. Maana unamlinda.
 
Ile timu ya lowasa, rostam, kalamagi.ingeachwa ingeleta ujinga mkubwa sana kwenye hii nchi.Hiyo ndio kazi ya wana usalama.

Hakukua na richimond wala nini. Mchezo tu ule.imetungwa movie na watu wakaikubali, muhusika kapewa hadi muda wa kujitetea lakini kashindwa kujitetea na watu wakaamini.

Dadadadeki..!!
 
Jana niliiona ile posting ya WikiLeaks. Nashukuru niliweza ku download PDF mbili,tatu kabla TISS hawapiga simu JF.
 
Sema jambawazi Jeikei
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…