Mzee Majuto na Ombi lake kwa Rais Kikwete

Hussein Massanza

JF-Expert Member
Joined
Dec 26, 2012
Posts
1,016
Reaction score
2,195
Akihojiwa katika Kipindi cha Mkasi cha EATV mwishoni mwa mwaka 2014, Msanii Mkongwe wa vichekesho na mchekeshaji bora zaidi aliyewahi kutokea Tanzania, Amr Athuman almaarufu kama Mzee Majuto, alitoa ombi lake la kununuliwa Trekta ili kuweza kumudu kuendesha maisha yake ya uzeeni kupitia kilimo baada ya kuachana na sanaa ya maigizo aliyoitumikia kwa zaidi ya miaka 20 sasa.

Kwa msisitizo mkubwa, Mzee Majuto alimwomba Rais wa JMT, Mhe. Jakaya Kikwete kama anamsikiliza, amsaidie kwenye hilo na atamshukuru sana kwani atamrahishia kutimiza ndoto zake, ambazo ni kupumzika nyumbani kwake Tanga pindi atakapostaafu kazi yake ya kuigiza!

''Kama ananisikiliza, Namwomba Mhe. Rais aninunulie gari ya kulimia, ili namimi eeh. niweze kupata walau kulima nikiwa mapumzikoni huko nyumbani, kwani ndoto yangu ni kuja kufanya kilimo nikiacha kazi hii ya sanaa''. Alisema Mzee Majuto katika kipindi cha Mkasi EATV.

Mtangazaji Salama Jabir, kwa udadisi alimuuliza Mzee Majuto kama anafahamu bei ya hilo Trekta, Naye kuonyesha ni kweli anahitaji alijibu kuwa alifuatilia na kujua ni takribani Sh. Milioni 25 za Kitanzania.

NB: Huu ni Ukumbusho tu kwa Mheshimiwa. Kama atajitolea kumsaidia, maana bila shaka ametingwa na mambo mengi na Muda wenyewe ndo huu wa lala salama!

 
Kumbe yuko smart majuto kujua kilimo kitamrahisishia maisha ya uzeeni
 
Mzee Majuto anaidai sanaa pesa nyingi sana...dunia haiko fair.
 
Mimi nilifikiri alivyo stafu kazi ndo akaingia kwenye sanaa? Kilimo kina hitaji nguvu ambazo sasa hivi hana. Kuna umri ukifika ni lazima upumzike tu.
 
Mzee majuto hakosi iyo pesa!
 
Kila mtu akimuomba Rais amnunulie trekta itakuwa vipi?

Kwa fursa alizozipata na anazoendelea kuzipata Majuto anaweza sana kununua trekta.
 
Nakumbuka ile siku Mzee Majuto ilibidi avae sura ya mbuzi kutoa ombi lake! Nakumbuka, dakika chache kabla Mzee Majuto hajatoa ombi hilo, Mzee Majuto akapewa za uso za jumla kwamba Long Time JK alikuwa anawa-feel sana wasanii, anawaita Ikulu na wakitoka hapo lazima watoke na bahasha lakini baadae, wasanii wakaanza tabia ya kupiga mizinga kwa JK na baadae JK akaamua kuwapotezea baada ya kuona mizinga imezidi...!!! Dah, ghafla tu Mzee Majuto nikaona amebadilika kabisa mzee wa watu, kumbe na mwenyewe alikuwa mbioni kupiga mzinga!!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…