Mzee Mkapa alitengeneza uongozi wa Nchi kwa ngazi mbalimbali

Mzee Mkapa alitengeneza uongozi wa Nchi kwa ngazi mbalimbali

dndagula

JF-Expert Member
Joined
Jul 24, 2016
Posts
1,602
Reaction score
1,650
Kwa maoni yangu wakati Hayati Mzee Mkapa akiingia madarakani mwaka 1995 alianza na Mikakati ya kuweka mifumo mbalimbali ambayo hadi sasa imekuwa endelevu. Kipindi hicho ndicho kiliibua Maboresho katika Utumishi wa Umma.

Hii iliendana na dhana ya ajira kwa kuzingatia sifa pamoja na kuibua viongozi wenye vipaji,weledi na wabunifu na wazalendo kwa ngazi mbalimbali za Taasisi za Serikali na Mashirika ya Umma.

Sheria ya Utumishi wa Umma Na 8 ya 2002 ilitungwa na miundo na mifumo ya kupandisha vyeo ilipitiwa. Viongozi wengi kuanzia ngazi ya Rais, Mawaziri, Makatibu wakuu, wakuu wa Idara za serikali walioko serikalini na waliostaafu salama na wachapa kazi wengi wao ni zao la Mkapa. (Mimi ni zao lake pia)Kipindi hiki tulifanya kazi kwa bidii na maarifa ili kufikia Malengo tena yanayopimika na kwa kuzingatia Sera Sheria kanuni na taratibu. Aidha,Mindset za wafanyakazi zilibadilishwa na dhana ya uwazi na ukweli

Ndiyo maana nimesema kipindi hiki kilikuwa cha kutengeneza Mifumo na Uongozi wa baadaye ndiyo maana tunao Mhesh Rais J Magufuli,Kikwete nk. ambao nao ni zao lake. Hivyo,TUMUOMBEE na kama ilivyo kwa viongozi wengine nashauri tuwe na MKAPA DAY kama kumbukumbu endelevu kwa Taifa ie Siku ya Utumishi wa Umma Public Service Day iitwe hivyo. RIP MZEE WETU.AMEN
 
Tuwekee na mifano ya viongozi mbalimbali waliotengenezwa kipindi cha Mkapa, ungeweka majina ingependeza zaidi.
 
Ni wengi kimsingi viongozi ngazi za kati na juu unaowaona 65% serikalini na wastaafu wa miaka 10 iliyopita wametokea kwenye mikono yake.
 
Kipindi hiki tulifanya kazi kwa bidii na maarifa ili kufikia Malengo tena yanayopimika na kwa kuzingatia Sera Sheria kanuni na taratibu. Aidha,Mindset za wafanyakazi zilibadilishwa na dhana ya uwazi na ukweli
Kwa kuisoma kwenye makaratasi kama hivi sasa, huu mstari mmoja na nusu, ni mambo yanayovutia kweli kweli.

Mkuu 'dndagula' sitaki kuonyesha kukusuta au kukulaumu wewe kwa kuandika mambo mazuri haya, lakini naomba pia nikuulize utueleze kama kweli haya yalifanyika huko maofisini, au yalikuwa ni mambo ya kwenye mafaili makabatini.

Hivi hawa wafanyakazi wenye urasimu waliolazimu Rais Magufuli "awanyooshe" alipochukua uongozi, nao hawa walianzia huko kwenye enzi hizo za Rais Mkapa? Na wale wafanyakazi hewa?

Siyaandiki haya kwa kubeza kazi alizofanya, kwa sababu alifanya kazi kisayansi na kwa taratibu mahsusi; lakini badala ya watu kutimiza kama ilivyotakiwa, wao wakabuni njia zao za kukwamisha utoaji wa huduma za serikali kwa wananchi.

Rais Magufuli amekija na njia zake tofauti ambazo hata kama hazitakuwa endelevu, lakini zinaonekana kuleta matokeo chanya.

Hebu jaribu kuyajadili haya kwenye mada yako hii.

Labda niongezee tu kama wazo lililoniijia baadae: Mambo/mipangomazuri/mizuri kama haya/hizi huhitaji ufuatiliaji wa karibu sana na kuifanyia tathmini mara kwa mara kuhakikisha kwamba malengo yaliyowekwa yamefikiwa na ufanisi unaendelea kupatikana.

Haya sio mambo ya kufanya kwa mara moja, au katika ngwe fulani basi na kuachia yajiendeleze yenyewe, hayataendelea, na ndio maana urasimu ulirudi mara tu baada ya semina na makongamano kufanyika.
 
Back
Top Bottom