Mzee Muta alivyomfunga miguu Saida Karoli

Pamoja sana mkuu. Ndo waamke sasa
Solo Thang alipasuka ya moyoni
Nashindwa kuelewa kwa mfano Msanii anatoa video ya Milioni 30. Na hana pesa iyo ya video iyo matokeo yake Lazima aingie katika mikataba iyo ya Kina chief Mangungo

Wasanii wanaangaika sana, Sema mameneja wawe na Roho ya kibinadamu wakati mwingine. Ivi mfano mtu kama Mutta anafurahia kuona Saida Kaloli anashindwa hata kwenda Studio kutoa hata nyimbo.

Hata kama ni bifu ifikie kipindi tuwe na ubinadamu, na kuthamini kile kitu ulichokivuna kutoka kwa mtu na isiwe ndio utaki hata kumuona ananyanyuka tena
 
Kwabahati nzuri gazeti lako halichoshi mkuu,,nimekuelewa sana..
 
Saida karoli ni dadangu na Muta Mutahba ni kak yangu....hawa ndugu zangu ni wajinga pengine kuliko wajinga wote Tanzanania niliowai kuwashuudia.
Hivi Muta na Ruge ni ndugu? Naomba nifahamishwe mkuu
 
Bora ingekuwa hivyo ulivyoandika. Mkataba wa Saida na Mzee Muuta umechukua haki zote za saidaa kwenye zile albam mbili za Chambua Karanga na Mapenzi kizunguzungu. Nyimbo zote kwenye Albam zile siyo za Saida ni za Fm Studiios alipewa hela kidogo akasign mkataba Mbovu.
 
Upo sawa Hakuna kiasi cha pesa kinachotosha kununua haki bunifu yoyote. Wanaohusika na haya ni Cosota siyo Basata Kama ulivyoandika ingawa mengi uliyosema ni sahihi sana.
 
Upo sahihi sana.
 
Wengi mtamlaumu Saida lakini ukweli ni kuwa "Saida karoli hakuwa na elimu wala hakupata mchangamano na watu ambao wangembadilisha kifikra "...

Huyu mama alitolewa kwenye upigaji wa ngoma vilabuni huko bukoba na tuzo yake pekee ilikuwa ni pombe... Hadi anakuja kuchukuliwa na hao walaghai na kuanza kumfanyisha matamasha ya kiasili , sidhani kama hata malipo kiduchu aliyolipwa yalimtoa ushamba kutokana na kuwa hakuizoea pesa "....

Hadi anakuja kuwa msanii mkubwa , yeye hakuijua thamani yake kabisa na alipokuja kushtushwa ndipo ukawa mwisho wake maana alitelekezwa mjini hadi akaanza kuuza chips.....

Mutta sidhani kama ana utu maana kwa pesa za kuujaza uwanja wa taifa ilipaswa amnufaishe japo kidogo...

Yote kwa yote... Tayari Saida amekwishajua wapi alipokosea hivyo, hapaswi kudai hadhi na haki yake kwa mdomo Bali kwa vitendo
 
Tumsaidie jamani Saida Si MTU wa kupanda Bajaji kwa kipaji cha sauti yake

Kwani bado yuko mjini au karudi kagera kulima ndizi

Nakumbuka interview yake moja saida akadai wimbo katengeneza video London akamalizia Uingereza!!!!
 
Hivi wasanii Fiesta wanalipwa ngapi?. Maana naskia malalamiko tu
 
Hata Late Kanumba FILAMU Zote ni Za The Game Quality na Steps Entertainment.
 
FELICIAN MUTA (FM) Alipelekeshana pia na JONGWE (SUGU ),Wanasheria wamsaidie Saida karoli.
 
Wakuu tuelewesheni kilichotokea maana tumevamia tu story katikati
 
Ndio maana mnasisitizwa Elimu Elimu Elimu, Mutta aliweza kuutumia ujinga wa Saida kama fursa

Mkuu wala hii sio fulsa ni utapeli....alafu alivyo mjinga kamtapeli mtu wa nyumbani.....kasahau msemo wa "zimwi likujualo halikuli likakwisha"....
 

Mutta ni intalahamwe.....utamwekeaje mtu mikataba ya kijinga kiasi hicho,yaani unajua kabisa mtu hajui na unajifanya kwamba anajua!!.
 
Hivi kumbe kina Rich Mavoko, Raymond na Harmonize wameliwa na WCB! Sijui kama wanalifahamu hili kwa undani kama ulivyoeleza.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…