Kwa kweli sijui kama ni Mzee kweli lakini hapa JF ni mtu ambaye amekuwa akitupa mchanganuo mzuri kuhusu masuala ya siasa.Uchambuzi wake kama kawaida kuna wakati ulikuwa unakera watu na kuna wakati uliwafurahisha wengi.
Kwa hoja zilizokuwa zinatolewa hapa inaelekea Mwanakijiji haishi ndani ya nchi ingawa ni Mtanzania.
Naamini ya kuwa katika kipindi hiki ambacho wengi tumejawa na uoga wa kuandika tunachokiamini angeweza kutusaidia kutupatia uchambuzi na kupunguza kutegemea twitter ambapo machapisho huwa mafupi.
Karibu Mwanakijiji na tuanze na haya,
Kwisha habari yake.
Mzee Mwanakijiji na Pasco kwa sasa ni sawa na wale vijana wa CCM Lumumba wanaolipwa buku saba kwa siku ili kufanya propaganda mitandaoni.
Wameshokwa mnoo humu JF.