Mzee Mwinyi awavunja mbavu waombolezaji Masasi; aeleza mara ya kwanza kuvaa viatu ilikuwaje

Mzee Mwinyi awavunja mbavu waombolezaji Masasi; aeleza mara ya kwanza kuvaa viatu ilikuwaje

fazili

JF-Expert Member
Joined
Jun 10, 2011
Posts
16,427
Reaction score
22,418


Baada ya Mzee Kikwete kuweka sawa mambo na kusema Mzee Mkapa hakupenda sifa pamoja na kufanya mambo mengi ambayo serikali hii bado wana jukumu la kuyakamilisha, mzee Mwinyi aliuchekesha umati wa waombolezaji kwa kuelezea jinsi alivyotoka mbali.

"Katika ujana wangu, nimevaa viatu mara mbili; mara ya kwanza wakati naenda jandoni, na mara ya pili nikiwa na miaka 13 baada ya kufanya kibarua cha kuchuma karafuu na kupata pesa. Ili viatu vyangu visichakae mapema, nilikuwa wakati mwingine navivua na kuvitundika begani huku nikitembea peku". Alisema Mzee Mwinyi.

Umati ulilipuka kwa kicheko na hii iliweka sawa mbavu za watu na kusaidia kuondoa huzuni baada ya zoezi la kumpunzisha Mzee Mkapa. Vijana tusikwame katika hali zetu duni za sasa, haya ni mapito tu na sio mwisho wa maisha yetu.
 
Tulisikia, hata usingetujazia mimaandishi yako humu. Local Channels zote zilirusha mazishi ya Mkapa, hata ile ya wanyama Safari channel.
 
Msemaji wa Serikali hajamjibu bado?

Hawachelewi kusema hili ni fumbo la kijembe kwa Magufuli.

Jando = Maadili

Kuvaa Viatu= Kuvaa dhamana ya uongozi.

Kuvibeba viatu visichakae = Kuuheshimu uongozi usiharibike.
 
Tulisikia, hata usingetujazia mimaandishi yako humu. Local Channels zote zilirusha mazishi ya Mkapa, hata ile ya wanyama Safari channel.
kwa vile ulisikia ama kuona wewe haimaanishi na wengine wote wameona pia. Hukuwa na sababu ya kuangalia kama ulishaangalia kabla.

Shukran kwa muanzisha uzi hata mimi ilikuwa sijaona.
 
Msemaji wa Serikali hajamjibu bado?

Hawachelewi kusema hili ni fumbo la kijembe kwa Magufuli.

Jando = Maadili

Kuvaa Viatu= Kuvaa dhamana ya uongozi.

Kuvibeba viatu visichakae = Kuuheshimu uongozi usiharibike.

Daaaaaa

Mwinyi huyuuu ambaye anataka JPM aongeze muda hana guts za kuongea hivyo......JK pekee ndio anaweza kumkosoa JPM
 
Mwinyi amevua viatu visichakae, baadhi tumevua viatu tuwe sawa na rafiki zetu ambao wazazi wao hawakua na uwezo wa kifedha kuwanunulia viatu.
 
Mwinyi amevua viatu visichakae, baadhi tumevua viatu tuwe sawa na rafiki zetu ambao wazazi wao hawakua na uwezo wa kifedha kuwanunulia viatu.
Asante kwa kunikumbusha hili nakumbuka nilivua viatu ili niwe sawa na wenzangu na tuweze kucheza mpira.
 
Daaaaaa

Mwinyi huyuuu ambaye anataka JPM aongeze muda hana guts za kuongea hivyo......JK pekee ndio anaweza kumkosoa JPM
Nazingua tu.

Mwinyi kajishusha hadhi sana.

Yani kama gari ilibaki na mafuta robo, sasa ineshuka kabisa imeenda kwenye E.

Naelewa sana kwa nini Nyerere alimpigia kelele sana.

Katoka hadhi ya urais kaporomoka kawa kama beki tatu mshamba.
 
Back
Top Bottom