Mzee Tanzania na Mama Mkubwa CCM

Mzee Tanzania na Mama Mkubwa CCM

clearmind

JF-Expert Member
Joined
Dec 26, 2013
Posts
813
Reaction score
1,913
Toka mzee wetu azaliwe na kubahatika kumpata mke wa kwanza wa kumtunza Februari 5, 1977 na kuwa mama wa Watanzania wote bara na visiwani kwa miaka mingi, hatimaye mwaka 1992, mzee kwa kushirikiana na mke mkubwa, aliweka wazi wazo lake la kuwa na wake wengi.

Wakaibuka wengi kwa namna ambayo haikutarajiwa NCCR MAGEUZI, CUF, CHADEMA, ACT WAZALENDO, DP, na wengine wengi huku kila mmoja akitamani kuwa katika mstari wa mbele wa kumlea mzee wetu Tanzania.

Wamefanya hivyo mara nyingi lakini nguvu ya mke mkubwa imekuwa haiwapi fursa ya kufurukuta na kufikia malengo kusudiwa katika malezi ya Mzee Tanzania.

Ni kipi kinachomfanya Bibi mkubwa kutotaka kuwapa wake wenza nafasi ya kumhudumia mzee?

Je, ni kweli ushawishi wa Bibi mkubwa kwa watoto wa Mzee Tanzania watokanao wake zake mbalimbali ni mkubwa kiasi cha kukubali yeye ndie amlee mzee kwa wakati wote?

Je, watoto wengi aliowazaa Bi mkubwa hawaoni kwamba nguvu zimemuishia na Mzee anahitaji kuendelea kupata huduma kutoka kwa wake zake wadogo?

Je, sisi watoto wa Mzee maoni yetu ni yapi tunapokaribia miaka mingine ya kuamua ni nani ashikilie malezi ya mzee?

Bi mkubwa atakuwa tayari kuwapa wake wenza majukumu ya kumlea mzee ambae wana historia ndefu ya maisha?
 
Mkuu

Hadi kitabu cha muongozo cha kukabidhiana majukumu kizaliwe Ndio mke mwenza atapenya kumhudumia Mzee!!

La sivyo hakuna chochote kitakacho endelea!

"Mzee warioba ajumuishwe kwenye kikosi kazi cha mkandala mchakato wa katiba mpya ukamilike mapema"
 
Mkuu

Hadi kitabu cha muongozo cha kukabidhiana majukumu kizaliwe Ndio mke mwenza atapenya kumhudumia Mzee!!

La sivyo hakuna chochote kitakacho endelea!

"Mzee warioba ajumuishwe kwenye kikosi kazi cha mkandala mchakato wa katiba mpya ukamilike mapema"
Asante sana kwa maono yako. Bi mkubwa anajiona kwamba bado ana nguvu ukizingatia kwamba kajipanga vilivyo kuhakikisha kwamba mzee anabakia mikononi mwake. Unadhani katiba inaweza kuwa na nguvu dhidi ya jeshi na vyombo vingine vya maamzi kama mama ndie atakaesimamia mchakato mzima?
 
Asante sana kwa maono yako. Bi mkubwa anajiona kwamba bado ana nguvu ukizingatia kwamba kajipanga vilivyo kuhakikisha kwamba mzee anabakia mikononi mwake. Unadhani katiba inaweza kuwa na nguvu dhidi ya jeshi na vyombo vingine vya maamzi kama mama ndie atakaesimamia mchakato mzima?
Takwa la katiba mpya Sio la mamkubwa ni la DOLA yenyewe!

Kwasababu DOLA ilionja joto la jiwe toka KWA house boy aliepita ambaye alikikanyaga kitabu na kuumiza WENGINE hadi member wa DOLA wakaona cha Moto!

Sasa mamkubwa kachoka na kuzeeka hana ujanja Hivyo atakabidhi kijiti KWA mke mwenza ambaye ni rafiki Ili asije poteza stahiki zake hapo katiba ikishapatikana!

Anashupaza shingo kiujanja ujanja lakini muda umefika wa yeye kukaa pembeni na mwaka huu ujao 2023 zipo dalili za WAZI kabisa zitaonekana,ni mwaka wa picha Mpya ya mwelekeo mpya,Mti utapukutisha majani Ili yachipue mengine mapya!
 
Takwa la katiba mpya Sio la mamkubwa ni la DOLA yenyewe!

Kwasababu DOLA ilionja joto la jiwe toka KWA house boy aliepita ambaye alikikanyaga kitabu na kuumiza WENGINE hadi member wa DOLA wakaona cha Moto!

Sasa mamkubwa kachoka na kuzeeka hana ujanja Hivyo atakabidhi kijiti KWA mke mwenza ambaye ni rafiki Ili asije poteza stahiki zake hapo katiba ikishapatikana!

Anashupaza shingo kiujanja ujanja lakini muda umefika wa yeye kukaa pembeni na mwaka huu ujao 2023 zipo dalili za WAZI kabisa zitaonekana,ni mwaka wa picha Mpya ya mwelekeo mpya,Mti utapukutisha majani Ili yachipue mengine mapya!
Ni muda wa kusubiri na kuona. Ikiwa watoto walio wengi kutoka kwa bi mkubwa nao wataunga mkono kupitia sanduku la siri, basi bila shaka tutashuhudia huduma mpya kwa mzee. Itahitajika nguvu ya ziada pia kufanya ushawishi kwa watoto wake hasa walioko vijijini ili kuona haya yakitokea.
 
Back
Top Bottom