Nashukuru mzee baba kwa mrejesho wako.
Ni kweli kule kwenye channel nasimulia movie baadhi tu, tena siku ambazo nakuwa na muda sababu natuma movies nyingi sana mzee baba, hivyo siwezi kuelezea kila mojawapo.
Nitajitahidi, lakini napata wazo la kuanzisha group lingine la Movies ambapo ntakuwa natuma movies ambazo tayari zina substitles ndani yake na pia maelezo yake kwa kina.
Lakini itakuwa na malipo madogo mkuu nami nipate hamasa.
Kuhusu Youtube, bado channel ni mpya, natoa video moja kwa juma, ndo maana unaziona zipo tatu tu. Lakini usijali, kadiri tunavyoenda ndivyo zinajaa...nipe muda.