Resilience
JF-Expert Member
- Jan 4, 2023
- 1,096
- 4,948
Kuna namna tulikosea katika mchakato wakuandaa viongozi. Wakina Mzee Warioba walipoamua kujiweka kando baada ya mwalimu kung'atuka ilikuwa kosa kubwa sana.
Nchi haikuhitaji urais wa majaribio tena bali ilitakiwa inapata viongozi kwa merits. Kinachoendelea sasa hivi toka amalize muda wake mzee Mwinyi tumekuwa tukipata viongozi kulingana na mazingira ya vita ya kisiasa yaliyopo mbele ya uwanja wa uchaguzi.
Kutokana na ukweli kwamba wanaopitishwa kuwa wagombea hawana nguvu kwa wapiga kura ndipo ikaingia kasumba kila mgombea uraisi anaaminishwa hana uwezo wakupita bila kupata backup ya dola.
Mzee Mkapa alisumbuliwa sana na Mrema hadi ikabidi mwalimu aingie kazini na yeye akakwama nakulazimisha kura za maruhani na majambia.
Mzee Kikwete alipoona Lowasa anamzidi nguvu akaweka mkakati wa kumfanya rafiki ndipo amalize kisiasa kwa kutumia dola. Vilevile kwa JPM na huko tuendako.
Ifike wakati tuanze kuandaa viongozi na kuwapa nafasi ya kujitangaza kwa umma itasaidia kufahamu nani anakubalika na kupunguza nguvu ya dola kwenye uchaguzi.
Nchi haikuhitaji urais wa majaribio tena bali ilitakiwa inapata viongozi kwa merits. Kinachoendelea sasa hivi toka amalize muda wake mzee Mwinyi tumekuwa tukipata viongozi kulingana na mazingira ya vita ya kisiasa yaliyopo mbele ya uwanja wa uchaguzi.
Kutokana na ukweli kwamba wanaopitishwa kuwa wagombea hawana nguvu kwa wapiga kura ndipo ikaingia kasumba kila mgombea uraisi anaaminishwa hana uwezo wakupita bila kupata backup ya dola.
Mzee Mkapa alisumbuliwa sana na Mrema hadi ikabidi mwalimu aingie kazini na yeye akakwama nakulazimisha kura za maruhani na majambia.
Mzee Kikwete alipoona Lowasa anamzidi nguvu akaweka mkakati wa kumfanya rafiki ndipo amalize kisiasa kwa kutumia dola. Vilevile kwa JPM na huko tuendako.
Ifike wakati tuanze kuandaa viongozi na kuwapa nafasi ya kujitangaza kwa umma itasaidia kufahamu nani anakubalika na kupunguza nguvu ya dola kwenye uchaguzi.