Mzize avunja ukimya pasi ya Chama, asema picha linakuja

Mzize avunja ukimya pasi ya Chama, asema picha linakuja

jjackline

Senior Member
Joined
Jul 25, 2024
Posts
111
Reaction score
274

Mshambuliaji wa Yanga, Clement Mzize amesema ubora wa pasi ya mwisho ya Clatous Chama ulimpa urahisi wa kukwamisha mpira nyavuni.

Mzize alifunga bao la nne na la mwisho kwenye ushindi wa mabao 4-1 ilioupata Yanga dhidi ya Azam katika fainali ya Ngao ya Jamii iliyochezwa juzi Jumapili kwenye Uwanja wa Mkapa, Dar es Salaam. Mabao mengine yalifungwa na Prince Dube, Yoro Diaby (alijifunga) na Stephane Aziz Ki. Bao la Azam lilifungwa na Feisal Salum 'Fei Toto'.

Akizungumza na Mwananchi, Mzize amesema kabla ya kuingia uwanjani akitokea benchi, Kocha Miguel Gamondi alimtaka kuhakikisha anatumia nguvu zote kupeleka mashambulizi kwa wapinzani na ndicho alichokifanya.

"Alinionyesha mianya mingi ya kupita na kunisisitiza kutumia nguvu na akili kusogeza mashambulizi kwa wapinzani ndicho nilichokifanya, bao nililofunga nilianza kulitengeneza mwenyewe kwa kukokota mpira kutoka eneo la mbali la uwanja," amesema na kuongeza;
Snapinsta.app_455364899_1488739915337981_7569661543213621925_n_1080.jpg

 
Nae amechoka sasa,,,Ameamua ajipakulie Minyama
 
Mimi nilifurahi tu kuona Azam Fc yenye Fei Toto ndani yake, inafungwa kwa mara nyingine tena na Yanga. Only that.
Tena goli nyingi!!! 😂😂😂😂.
Hata hivyo Yanga second half waliamua kuwastah sana Azam. Waliamua kutowavunjia heshima vinginevyobhali ingekua mbaya kuliko
 
Kwahiyo zile poor finishing zake za siku zoote anataka kusema hakua anaoeea mipasi ya diZain ya Chama
 
Chama ulikuwa mfalme simba leo umeenda kuwa raia wa kawaida utopoloni
Kweli mkataa pema pabaya panamuita.
Naniatakupa heshima huko kama uliyopewa simba?
Huko wana wafalme wao.
 
Back
Top Bottom