Mzizima Derby (Simba, Azam) yahamishwa uwanja, kupigwa Benjamin Mkapa

Mzizima Derby (Simba, Azam) yahamishwa uwanja, kupigwa Benjamin Mkapa

Waufukweni

JF-Expert Member
Joined
May 16, 2024
Posts
2,060
Reaction score
5,648
Bodi ya Ligi Kuu Tanzania (TPLB) imebadili uwanja na muda wa kuanza kwa mchezo namba 167 wa Ligi Kuu ya NBC baina ya Simba na Azam ambao ulipangwa kufanyika kwenye Uwanja wa KMC Complex, Februari 24,2025 kuanzia saa 10:00 ambapo sasa utafanyika katika Uwanja wa Benjamin Mkapa siku hiyohiyo kuanzia saa 1:00 usiku.
IMG_3224.jpeg

Taarifa iliyotolewa na TPLB leo imesema kuwa sababu ya mabadiliko hayo ni kutoa fursa kwa mashabiki wengi kutazama.
IMG_3228.jpeg

"Sababu ya mabadiliko hayo ni kutoa nafasi kwa mashabiki wengi zaidi kuhudhuria mchezo huo ambao ni moja ya michezo mikubwa ya Ligi Kuu ya NBC inayovuta hisia za watu wengi.

"Uwanja wa Benjamin Mkapa wenye uwezo wa kuingiza mashabiki 60,000 umekuwa ukitumika kwa michezo mingi mikubwa na inayohusisha mashabiki wengi zaidi."
IMG_3227.jpeg
 
Hakika mechi hiyo ina hadhi ya uwanja kama huo.
Na hasa kama uwanja huo haujafungwa kwa shughuli nyingine
 
Uamuzi sahihi. Watu wangebanana sana pale Mwenge na labda hata maafa yangeweza kutokea. Kuna mechi hasa za Simba automatically inabidi zichezwe uwanja mkubwa siyo suala la kusubiri kuangalia upepo umekaaje.

Mechi ya Yanga na Azam ni ndogoo saaana ndiyo maana ilichezwa kule Chamazi.
 
Bodi ya Ligi Kuu Tanzania (TPLB) imebadili uwanja na muda wa kuanza kwa mchezo namba 167 wa Ligi Kuu ya NBC baina ya Simba na Azam ambao ulipangwa kufanyika kwenye Uwanja wa KMC Complex, Februari 24,2025 kuanzia saa 10:00 ambapo sasa utafanyika katika Uwanja wa Benjamin Mkapa siku hiyohiyo kuanzia saa 1:00 usiku.
View attachment 3245378
Taarifa iliyotolewa na TPLB leo imesema kuwa sababu ya mabadiliko hayo ni kutoa fursa kwa mashabiki wengi kutazama.
View attachment 3245386
"Sababu ya mabadiliko hayo ni kutoa nafasi kwa mashabiki wengi zaidi kuhudhuria mchezo huo ambao ni moja ya michezo mikubwa ya Ligi Kuu ya NBC inayovuta hisia za watu wengi.

"Uwanja wa Benjamin Mkapa wenye uwezo wa kuingiza mashabiki 60,000 umekuwa ukitumika kwa michezo mingi mikubwa na inayohusisha mashabiki wengi zaidi."
View attachment 3245380
Sunche na Kapeto, side na said bila kusahau backup ya refa.
 
Simba A vs Simba B. Moja kwa moja Simba A lazima ashinde.
 
Back
Top Bottom