Mzumbe university

Yusuph p. Kisunzu

Senior Member
Joined
Dec 21, 2012
Posts
120
Reaction score
9
Habari wana Jf samahanini wa mjengo,naomba msaada kwa anayefahamu zaidi juu ya namna ya kujiunga na MZUMBE University kwa faculty ya Public Health Management ukiwa na kozi yoyote ya afya hasa kwa Clinical Assistant.
 
Ingia kwenye website yao unaweza kukuta fomu. Ikishindikana omba kupitia TCU.
 
Clinical Assistance unamaana ni ngazi ya certificate?
Ila kama ni mtumishi yeyote wa kada ya Afya na ukiwa na Ufaulu ule wa Daraja B kwa maana Diploma GPA ya 2.7 mpaka 5 unaruhusiwa kusoma kozi hiyo!! Kama ni Diploma holder na una GPA ya kutosha kusoma chuo kikuu Ruksa !
 

nashukuru sana umenifumbua macho.
 
Mzumbe University, hakuna faculty ya Public Health Management. Ila kuna shule kuu ya utawala na uongozi yaani School of Public Administration and Management. (SOPAM). Moja kati ya Idara zinazounda Shule ile ni Health Services Management na sio Public Health Management.

Hata hivyo, nashindwa kukushauri kwa kuwa hujasema hiyo kozi ya Clinical Assistant ni Certificate, Diploma au Advanced Diploma?

Kwa level ya Bachelor in Health Services Management ukiwa na Diploma in Health related field utakuwa unaqualify.
 

hiyo Clinical Assistant ni Certificate kwa kuzingatia ile sifa ya any medical related course.
 

Kaka samahani ni Health service Management Ama Health system Management
 
Kwa undegraduate ni Health Services Management ila kwa level ya Masters ni Health Systems Management.
 
Kwa kigezo cha certificate, hujaqualify kusoma Bachelor of Public Administration (BPA)-in Health Services Management(HSM). Jaribu kuanza na Diploma then utaendelea kaka. Kila laheri.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…