Mzunguko wangu haswa ni upi?

Mzunguko wangu haswa ni upi?

mchoyo

Member
Joined
Aug 13, 2013
Posts
48
Reaction score
8
Habari na poleni na majukumu ya kulijenga taifa,

Kama kichwa cha habari kilivyojieleza hapo juu naombeni msaada wenu wa kunijuza hiki kitu kinanitatiza nashindwa kuujua mzunguko wangu kwa ujumla.

Mwezi wa saba niliingia tarehe 9 mwezi na wa nane tarehe 5 but wa tisa tarehe 3 bado sijaelewa na tarehe zipi mimi napata pregnant maana nahitaji mtoto kwa sasa. Ni hayo tu.

Asanteni.
 
Kwa inavyoonyesha wewe mzunguko wako ni wa siku 27-29; kwa sababu kutoka tar 9 july mpaka 4 august ni siku 27, na kutoka tar 5 august mpaka tar 2 sept ni siku 29.
Siku unayoanza kupata hedhi ndo siku ya kwanza katika kuhesabu mzunguko wako.
Ukitaka upate mimba inabidi ukutane na mwanaume kati ya siku ya 11 mpaka 18 ndo kunakuwa na uwezekano mkubwa wa mimba kutunga kwa sababu yai la mwanamke linapevuka kati ya siku ya 12-16.
 
Kutokana na maelezo yako nimeweza kupata information ifuatayo:
9 July - 4 August (27 Days)

5 August - 2 September (29 Days)

3 September - 29/30 September au 1 October (27, 28, 29 Days)

Kutokana na information hizo ni wazi kuwa mzunguko wako hauna kasoro zozote na ni wa kawaida wenye wastani wa siku 28.

Sasa bi mkubwa mchoyo labda nikuulize swali, unatarajia upate ujauzito mwezi gani?

Kama ni mwezi huu wa September basi shirikiana kimapenzi na mumeo kuanzia tarehe 13 hadi tarehe 20 maana hapo katikati ndipo siku za hatari ziangukiapo...
 
asante sana kwa msaada wako nimeplan mwez huu wa tisa nitafata ulichonielekeza then ntakuja kukupa feedback asante mungu akubariki huendelee kutupatia hiyo elimu
 
asante sana kwa msaada wako nimeplan mwez huu wa tisa nitafata ulichonielekeza then ntakuja kukupa feedback asante mungu akubariki huendelee kutupatia hiyo elimu

Ubarikiwe pia ila kuna elimu ambayo nadhani unahitaji kuijua na hushauriwa kwa mwanamke anayetaraji kushika ujauzito.

Hakikisha kuwa kabla ya yote unakwenda hospitali na kufanyiwa vipimo ili kujua kama afya yako iko salama au la kwa ajili ya kushika mimba.

Vifuatavyo ni baadhi ya vipimo vinavyoshauriwa kufanywa:

1. General examination au uchunguzi wa jumla.
2. Kipimo cha kensa au Pap smear.
3. Kipimo cha magonjwa ya zinaa (STD) kama vile Chlamydia ambayo huweza kuathiri uwezo wako wa kushika mimba.
4. Kipimo cha damu cha kuangalia kama una upungufu wa damu, Rh na kinga yako ya mwili dhidi ya ugonjwa wa Rubella.
5. Kipimo cha mkojo cha kuchunguza iwapo una ugonjwa wa kisukari.
Ugonjwa wa kisukari huweza kumzuia mtu asishike mimba hata iwapo mzunguko wake wa mwezi uko sawa, anapata Ovulation na kidhahiri anaonekana hana tatizo lolote.
6. Kama una paka nyumbani au unakula sana nyama (red meat) pengine si vibaya pia kupima kipimo cha Toxopmasmosis infection.
7. Kuyajua na kuzingatia baadhi ya mambo yanayoathiri kushika mimba ambayo ni pamoja na:-
• Ingawa unene unaweza kumzuia mtu asishike mimba lakini kufanya mazoezi sana na kuwa na uzito mdogo sana wa zaidi ya kilo 50 huweza pia kumsababisha mtu asishike mimba. Mazoezi ya kupindukia pia huathiri homoni mwiilini.
• Kuwa na fikra nyingi na msongo wa mawazo 'stress' huweza pia kauthairi uwezo wa mtu wa kushika mimba.
• Kutokula vizuri na kutopenda kula kwani humkosesha mwanamke au hata mwanamme baadhi ya virutubisho muhimu vinavyotakiwa kwa ajili ya kufanikisha suala la kushika mimba.
• Sigara, marijuana na pombe ni miongoni mwa vitu ambavyo vinaweza kuathiri uwezo wa kubeba mimba.

Na mengineyo mengi ambayo ukifika hospitali utashauriwa ikiwemo na matumizi ya virutubisho kadha wa kadha kama matumizi ya vidonge vya Folic
 
asante damu nilipima fbp (full blood picture) iksgundulika nina high prolactin but walinipa dawa aina ya bramestone 2.5 gm na kuna dawa imeandikwa one daily women pia pioglitazone hydrochloride tables 30gm
 
mzunguko uko sawa hauna tatizo kama unahitaji la kupata ujauzito better days ni 13 up to 19, mwez huu kila la kher
 
asante MankaM nitafata ushauri wenu wote kwa ujumla
 
Me ningekushauri jitahidi kumate na mumewe kuanzia trh 11 hadi 19 ili possibility ya kupata mimba iwe kubwa zaidi. Kama mwezi huu utakua unamzunguko wa siku 27 basi trh13 ndio siku ambayo kunauwezekano mkubwa wa yai kupevuka kama utakuwa siku29 basis trh15 ndio siku ambayo kunauwezekano mkubwa wa yai kupevuka
 
Pia kati ya trh11 hadi 19 kuna siku utahisi unaham kubwa ya kusex kuliko kawaida pia joto la mwili litaongezeka kidogo ukiona dalili kama hizo kati ya izo trh hapo basi jua ndo muda mwafaka wa wewe kukutana na mwezako kwn kutakua na great chance ya siku hiyo kuwa ndo siku muhimu zaidi kwa ajili ya wewe kupata ujauzito
 
duh ngoja hizo siku mwenzangu anazozililia MIMI NIZIKIMBIE KAMA UKOMA kwa sasa lakini
 
sasa kama mzunguko wangu 27 na 29 bac nianze kusex kuanzia cku ya 13-20 hapo vp siku nzur kabisa inamaana 13 ndo uwezekano upo mkubwa c ndio
 
Back
Top Bottom