Mkalukungone mwamba
JF-Expert Member
- Aug 29, 2022
- 862
- 1,755
Kocha wa Kaizer Chiefs, Nasreddine Nabi alikuwa hapa nchini kwa siku mbili kisha kufanya vikao na mabosi wa Yanga aliowahi kufanya nao kazi kwa mafanikio lakini amewaambia mabosi hao kuwa anaamini Yanga itacheza nusu fainali ya Ligi ya Mabingwa Afrika msimu huu.
Nabi amefanya kikao na Mfadhili wa klabu hiyo, Gharib Said Mohammed, Rais Injinia Hersi Said pamoja na Mjumbe wa Baraza la Wadhamini, Anthony Mavunde kisha akawaambia kama ni timu basi msimu huu wanayo.
Kocha huyo raia wa Tunisia amesema kuwa kwa kikosi ambacho Yanga inacho msimu huu ni kizito ambacho sio tu kutinga makundi, lakini kama ikivuka hapo basi itakwenda hadi nusu fainali itategemea na mpinzani gani watakutana naye.
"Nimekutana na viongozi wa Yanga tumekuwa na vikao vizuri vya kifamilia, nilifanya kazi hapa, bado nina maelewano mazuri na viongozi lakini pia wachezaji hata mashabiki na wanachama.
"Nimefurahia kuona kila ninapopita bado watu wanakumbuka kuhusu Nabi, watu wa Yanga, Simba na hata timu nyingine, nimewaambia viongozi kuwa wana timu nzuri sana msimu huu, sitashangaa kama watavuka mbali zaidi ya hatua ya makundi kwa kucheza robo fainali na hata nusu fainali.
"Nadhani ni timu chache zinaweza kuwa na kikosi kizito kama hiki cha Yanga, naamini watafanya vizuri sana hapa ndani na hata Afrika."
Soma Pia: Utabiri: Msimu wa 2024-25, zote Simba na Yanga zitafika fainali za mashindano ya CAF
Aidha Nabi alisema mbali na kuwa na timu bora pia kocha wao Miguel Gamondi mbinu zake zimeongeza ubora mkubwa wa timu hiyo ambayo aliifundisha kwa misimu miwili.
"Sio tu kikosi lakini hata benchi la ufundi ni zuri, nimekutana nao, wana kocha bora sana ambaye falsafa zake zimeipa nguvu zaidi timu hili nalo ni muhimu sana," alisema kocha huyo.
Yanga tayari imeshaweka mguu mmoja ndani kutinga hatua ya mtoano kuwania kufuzu makundi baada ya kushinda ugenini kwa mabao 4-0 dhidi ya Vital'O ya Burundi.
Nabi amefanya kikao na Mfadhili wa klabu hiyo, Gharib Said Mohammed, Rais Injinia Hersi Said pamoja na Mjumbe wa Baraza la Wadhamini, Anthony Mavunde kisha akawaambia kama ni timu basi msimu huu wanayo.
Kocha huyo raia wa Tunisia amesema kuwa kwa kikosi ambacho Yanga inacho msimu huu ni kizito ambacho sio tu kutinga makundi, lakini kama ikivuka hapo basi itakwenda hadi nusu fainali itategemea na mpinzani gani watakutana naye.
"Nimekutana na viongozi wa Yanga tumekuwa na vikao vizuri vya kifamilia, nilifanya kazi hapa, bado nina maelewano mazuri na viongozi lakini pia wachezaji hata mashabiki na wanachama.
"Nimefurahia kuona kila ninapopita bado watu wanakumbuka kuhusu Nabi, watu wa Yanga, Simba na hata timu nyingine, nimewaambia viongozi kuwa wana timu nzuri sana msimu huu, sitashangaa kama watavuka mbali zaidi ya hatua ya makundi kwa kucheza robo fainali na hata nusu fainali.
"Nadhani ni timu chache zinaweza kuwa na kikosi kizito kama hiki cha Yanga, naamini watafanya vizuri sana hapa ndani na hata Afrika."
Soma Pia: Utabiri: Msimu wa 2024-25, zote Simba na Yanga zitafika fainali za mashindano ya CAF
Aidha Nabi alisema mbali na kuwa na timu bora pia kocha wao Miguel Gamondi mbinu zake zimeongeza ubora mkubwa wa timu hiyo ambayo aliifundisha kwa misimu miwili.
"Sio tu kikosi lakini hata benchi la ufundi ni zuri, nimekutana nao, wana kocha bora sana ambaye falsafa zake zimeipa nguvu zaidi timu hili nalo ni muhimu sana," alisema kocha huyo.
Yanga tayari imeshaweka mguu mmoja ndani kutinga hatua ya mtoano kuwania kufuzu makundi baada ya kushinda ugenini kwa mabao 4-0 dhidi ya Vital'O ya Burundi.