Nabii ajitokeza kumtabiria Kenyatta urais wa Kenya, ni yule aliyemtabiria Kibaki

Nabii ajitokeza kumtabiria Kenyatta urais wa Kenya, ni yule aliyemtabiria Kibaki

Bishop Hiluka

JF-Expert Member
Joined
Aug 12, 2011
Posts
7,147
Reaction score
14,699
Nabii mashuhuri anayeibukia wa Venezuela, Dionny Báez, amebainisha kuwa
Mungu amemuonesha kuwa rais wa nne wa Kenya. Mwaka 2007, nabii huyo
alibashiri kwamba Kibaki angerejea katika urais na akawa sahihi. Wakati huu,
anaamini kuwa atakuwa sahihi tena. Katika ujumbe wa kinabii alioutoa mnamo
Desemba 2, 2012, uliowekwa Youtube, Báez aliwaambia waumini, jijini Nairobi,
kwamba Mungu amemwonesha kwamba Kenya itampata rais wake ajaye kutoka
Mlima Kenya. Alisema: "Wenye masikio watasikia, Bwana anasema, mtaangalia
mlima mrefu zaidi na kumpata rais wenu ajaye."

Mlima Kenya ulio eneo la Kati ya Kenya kuna watu watatu wanaogombea urais
katika uchaguzi wa mwaka huu, Uhuru Kenyatta, Martha Karua na Peter Kenneth.
Ingawa nabii huyo hakufafanua maelezo yake, wachambuzi wa siasa wanasema
kuwa uhakika wa Martha Karua na Peter Kenneth kushinda haupo kabisa, kwa maana
hawana ushawishi hata katika vitongoji vyao wenyewe. Hii ina maana kwamba
Mtume Báez alikuwa anazungumza juu ya Uhuru Kenyatta kuwa rais wa nne wa Kenya.

Nabii huyo alitabiri kuwepo kwa ghasia nyingine za baada ya uchaguzi, safari hii
zikijumuisha silaha kali zaidi na bunduki kutumika. Hata hivyo alisema kuwa vurugu
zitakuwa na athari ndogo kuliko za 2007/8.

Nakumbuka hapa kwetu, EL ameshatabiriwa na TB Joshua kuwa rais wa tano wa TZ,
na sasa yanatokea huko Kenya, sijui imekaaje hii ya wanaojiita manabii kujiingiza
katika kuwatabiria wanasiasa?...
 
Amekosea sana,urais upo mbali sana na huyu jamaa!
 
ALOKWAMBIA TB JOSHUA KAMTABIRIA EL NI NANI? you tube imeandikwaje usije leta habari za vijiweni
 
ALOKWAMBIA TB JOSHUA KAMTABIRIA EL NI NANI? you tube imeandikwaje usije leta habari za vijiweni
Mbona unapanic, kwani unaamini katika utabiri kwa kuhisi
kuwa mtu wako atabwagwa? Be cool mamen...
 
mtume na nabii wamejaa wengi kweli....muda si mrefu watajitokeza watakaojiita Mungu muumba na mijitu itawaabudu
 
nabii mashuhuri anayeibukia wa venezuela, dionny báez, amebainisha kuwa
mungu amemuonesha kuwa rais wa nne wa kenya. Mwaka 2007, nabii huyo
alibashiri kwamba kibaki angerejea katika urais na akawa sahihi. Wakati huu,
anaamini kuwa atakuwa sahihi tena. Katika ujumbe wa kinabii alioutoa mnamo
desemba 2, 2012, uliowekwa youtube, báez aliwaambia waumini, jijini nairobi,
kwamba mungu amemwonesha kwamba kenya itampata rais wake ajaye kutoka
mlima kenya. Alisema: "wenye masikio watasikia, bwana anasema, mtaangalia
mlima mrefu zaidi na kumpata rais wenu ajaye."

mlima kenya ulio eneo la kati ya kenya kuna watu watatu wanaogombea urais
katika uchaguzi wa mwaka huu, uhuru kenyatta, martha karua na peter kenneth.
Ingawa nabii huyo hakufafanua maelezo yake, wachambuzi wa siasa wanasema
kuwa uhakika wa martha karua na peter kenneth kushinda haupo kabisa, kwa maana
hawana ushawishi hata katika vitongoji vyao wenyewe. Hii ina maana kwamba
mtume báez alikuwa anazungumza juu ya uhuru kenyatta kuwa rais wa nne wa kenya.

Nabii huyo alitabiri kuwepo kwa ghasia nyingine za baada ya uchaguzi, safari hii
zikijumuisha silaha kali zaidi na bunduki kutumika. Hata hivyo alisema kuwa vurugu
zitakuwa na athari ndogo kuliko za 2007/8.

Nakumbuka hapa kwetu, el ameshatabiriwa na tb joshua kuwa rais wa tano wa tz,
na sasa yanatokea huko kenya, sijui imekaaje hii ya wanaojiita manabii kujiingiza
katika kuwatabiria wanasiasa?...

hao ni manabii wa uwongo! Mungu humchagua mtu.....mimi naweza kusema ni macampeignist!
 
nani alikuambia Kabaki alishinda? acha mambo yako tatizo hamtaki na wengine waongoze nchi mnafikiri kuwa kenya is only for Kikuyu, shame on you plus huyo mtabiri wako.

Mbona umenishambulia hivi jamani? Narudia :Utabiri wa hivi ni kazi ya shetani
 
...............
Nakumbuka hapa kwetu, EL ameshatabiriwa na TB Joshua kuwa rais wa tano wa TZ,
na sasa yanatokea huko Kenya, sijui imekaaje hii ya wanaojiita manabii kujiingiza
katika kuwatabiria wanasiasa?...

Bishop Hiluka na wengine mnaoamini kwa kusoma na kusikia toka kwa source mbalimbali kuwa eti "TB Joshua alimtabiria Mheshimiwa Lowasa kuwa Raisi wa Tano Tz", ninaomba niwatahadharishe.

Habari hiyo ni ya uwongo mweupe kwa vigezo vifuatavyo;-
  1. T.B Joshua atoapo utabiri unaoihusu nchi au taifa au dunia hua hautoi chumbani au kwenye vyumba vya hoteli (kama mikataba ya Tz inavyosainiwa). Bali hutoa hadharani na huonekana live kupitia Emmanuel TV. -Huu haukuonekana japo wapo maelfu ya Watz waliangalia live Lowasa alipokuwa pale kanisani kwa siku zote.
  2. Utabiri huo utarudiwa tena na tena. -Huu toka utajwe/usemwe kuwa ulitokea haujawahi kurudiwa hata leo.
  3. T.B Joshua hana tabia ya kujipendekeza kwa kiongozi yeyote japo anamheshimu kila mtu na Kanisa lake huwajali watu wote wanaofika pale pasi na vyeo vyao. -Hakuna uspesheli wa Lowasa kuwepo kwenye ibada ile bali ni binadamu kama wengine tu wanaomtafuta Mungu.
  4. Vile vinyaraka vilivyoleta habari hii (vilivyopatikana bungeni) ni vya "PRO-LOWASA" -Kumbuka ni nani na nani walikuwa wakibadilishana jumbe na hata leo msimamo wao juu ya "kundi wanalolisupport".
Mengine mnaweza kuongezea.
 
hata kibaki hakushinda. basi yupo sahihi kama katabiri hivyo kwa kenyatta pia.
 
ALOKWAMBIA TB JOSHUA KAMTABIRIA EL NI NANI? you tube imeandikwaje usije leta habari za vijiweni

Mkuu mbona nabii Joshua aliwahi kutabiri kwamba OBAMA atashindwa kuchaguliwa katika kipindi cha pili cha urais!
 
Huyo nabii alitakiwa kutabiri kuwa Kibaki angeshinda kwa kuiba kura
 
Hata bila utabiri, ni rahisi kusema Uhuru atashinda. Uhuru ni candidate anayependwa Kenya, hasa WAKIKUYU ambao hawataki hadi leo kutawaliwa na kabila jingine.

Tusubiri tuone, hata mie naweza kutabiri kuwa MUDAVADI na KARUA HAWATASHINDA!!!!!!!
 
Nabii mashuhuri anayeibukia wa Venezuela, Dionny Báez, amebainisha kuwa
Mungu amemuonesha kuwa rais wa nne wa Kenya. Mwaka 2007, nabii huyo
alibashiri kwamba Kibaki angerejea katika urais na akawa sahihi. Wakati huu,
anaamini kuwa atakuwa sahihi tena. Katika ujumbe wa kinabii alioutoa mnamo
Desemba 2, 2012, uliowekwa Youtube, Báez aliwaambia waumini, jijini Nairobi,
kwamba Mungu amemwonesha kwamba Kenya itampata rais wake ajaye kutoka
Mlima Kenya. Alisema: "Wenye masikio watasikia, Bwana anasema, mtaangalia
mlima mrefu zaidi na kumpata rais wenu ajaye."

Mlima Kenya ulio eneo la Kati ya Kenya kuna watu watatu wanaogombea urais
katika uchaguzi wa mwaka huu, Uhuru Kenyatta, Martha Karua na Peter Kenneth.
Ingawa nabii huyo hakufafanua maelezo yake, wachambuzi wa siasa wanasema
kuwa uhakika wa Martha Karua na Peter Kenneth kushinda haupo kabisa, kwa maana
hawana ushawishi hata katika vitongoji vyao wenyewe. Hii ina maana kwamba
Mtume Báez alikuwa anazungumza juu ya Uhuru Kenyatta kuwa rais wa nne wa Kenya.

Nabii huyo alitabiri kuwepo kwa ghasia nyingine za baada ya uchaguzi, safari hii
zikijumuisha silaha kali zaidi na bunduki kutumika. Hata hivyo alisema kuwa vurugu
zitakuwa na athari ndogo kuliko za 2007/8.

Nakumbuka hapa kwetu, EL ameshatabiriwa na TB Joshua kuwa rais wa tano wa TZ,
na sasa yanatokea huko Kenya, sijui imekaaje hii ya wanaojiita manabii kujiingiza
katika kuwatabiria wanasiasa?...

wewe unayejiita Bishop Hiluka, wewe ni mkristo? nadhani wewe si mkristo. nenda kasome biblia na ujifunze jinsi manabii walivyokuwa karibu na kuhusika na watawala. pia waliwatabiria ni nani atakuwa mfalme na nani amekataliwa. sasa unaonekana wewe ni mkristo kwa kuzaliwa tu. Siasa ziliasisiwa na Mungu. Usipost vitu usivyovielewa.
 
Manabii wanasema ukweli hata jk alitabiriwa akawa sasa lowasa naye atakuwa
 
wakati mwingine utabari huwa kinyume. Mtabiri huonesha kushinda kwa mtu kumbe alikusudia ausome kinyume na anavyoona na kwa kutokutambua hili mtabiri akabugi. Rejea utabiri wa Kakobe enzi ya Lyatonga.
 
Kwani Kibaki alishinda,si alikwiba kura na ndio maana akaapishwa kama mwizi usiku na hao akina Karua,kama huo ndio utabiri basi kwa mara ingine tena huyo aliyetabiriwa atashinda kwa kukwiba kura
 
wewe unayejiita Bishop Hiluka, wewe ni mkristo? nadhani wewe si mkristo. nenda kasome biblia na ujifunze jinsi manabii walivyokuwa karibu na kuhusika na watawala. pia waliwatabiria ni nani atakuwa mfalme na nani amekataliwa. sasa unaonekana wewe ni mkristo kwa kuzaliwa tu. Siasa ziliasisiwa na Mungu. Usipost vitu usivyovielewa.

Kwa vyovyote utakuwa na matatizo ya akili, hiki nilichoandika hapa
kinahusiana nini na ukristo? Mbona unataka kudandia treni kwa mbele!
Kumbuka si mimi niliyetunga haya bali yameshaandikwa na magazeti
na mitandao ya Kenya ambayo mimi pia nimesoma na kuyaripoti hapa
ili watu wengine wasome. Huo ukristo unaouongelea wewe unanihusu
nini mimi? I don't give a shit!...
 
Back
Top Bottom