Nabii Mkuu Dkt. GeorDavie ameweka wazi kuwa ametoa magari takriban 200 kwa waumini wake kama sehemu ya kuwasaidia kiuchumi na kiimani. Akizungumza katika mahojiano na Salim Kikeke, alisema kuwa magari hayo hayahitaji matangazo yoyote ya wazi, bali waumini wanaohitaji huambiwa wapi waende kuyachukua.
"Magari niliyotoa kwa waumini yanafikia karibu 200. Hizo sihitaji kutangaza popote. Anapokuwa na uhitaji, anaelekezwa kwa mtu fulani na kwenda kuchukua." alisema Nabii GeorDavie.