Nadai fedha- nasingiziwa kuwa nilipewa-naomba msaada wa kisheria

Mrekebishaji

Senior Member
Joined
Mar 19, 2009
Posts
168
Reaction score
63
Nilikuwa nisafiri kwa shirika fulani la ndege toka Dar kwenda Nairobi. Nikaahirisha safari. nikatoa taarifa airport mahali nilipolipia na kuwaambia nimeshindwa kusafiri, wakasema tiket itakuwa wazi mpaka mimi nikithibitisha kuwa nasafiri lini ndio wataweka tarehe hiyo. ilikuwa June 28, 2012. kesho yake, baada ya kuona sitasafiri tena nikaenda ofisini kwao na kujaza form ya kuomba kurudishiwa fedha. Niliambiwa huchukua wiki tatu na nilijua hivyo. zikapita wiki tatu, kila nilipofuatilia naambiwa mhasibu hayupo, baada ya muda mrefu kupita, mara mhasibu akasema claim yangu imekwama, madai yangu yamekuwa labelled 'Void'. Baada ya kufuatilia nikaambiwa kuwa yule mtu wa airport aliandika kuwa mimi nilirudishiwa fedha palepale. KITU AMBACHO SI KWELI. nikaambiwa nifuatilie kwa Finance Manager wao. nilikutana nae, akasema ni nimpe maelezo ilivyokuwa. Akasema nimtumie email maelezo yangu. then akanijibu kuwa niseme lini nitaenda nikutane na boss wao mwingine. Siku nikaenda, nikawekwa 'KITIMOTO' katikati ya watu kama nane hivi. wakanihoji, kwa ufupi ni kama mtuhumiwa. Nikaeleza ukweli kuwa mimi sikurudishiwa fedha, lakini pia nilishangaa sana shirika kubwa, eti aiport mtu akighairi safari wanaweza kurudisha fedha palepale na staff wao anasema mimi alinirudishia, nikasema ina maana hamna sehemu ya mtu anaposaini kuwa amerudishiwa wakasema hawafanyi hivyo,ila wanakati ticket kwenye system basi. NIKASHAANGA SAAAAANA. Haihitaji uhasibu kujua hapo ni kosa huwezi kuwa na mfumo unarudisha fedha bila mtu kusaini kuwa amepokea. wakakiri kosa. Niliwaambiwa hiyo itatoa fursa kwa wafanyakazi wao kufanya utapeli kuwa wamewarudishia fedha watu kumbe si kweli, a mteja hawezi kuangalia computer yao na kuona umeandikiwa umelipwa kumbe si kweli. Wakasema itabidi waombe camera za aiport ili zionyeshe kama nilirudishiwa fedha au la. Baada ya kama wiki tatu nikapigiwa simu na watu wa 'usalama' wao wakinihoji. Lakini mpaka sasa ni kama wiki tatu zimepita tena kimya. Nimeandika email mbili sijajibiwa. Zaidi ya laki tano. UKWELI ni kuwa sasa imepita miezi minne na sijui hatma yangu. Naomba ufafanuzi wa kisheria. Moja nimetuhumiwa kuwa ni kama tapeli wakati si kweli, tunangoja ushauri. lakini pia fedha yangu kukaa huko kwa zaidi ya miezi 4 ni hasara kubwa, na wote tunajua. USHAURI WENU PLSE.
 
Mkuu hapo una kila haki ya kufungua kesi ya madai ili kupata haki yako pamoja na usumbufu ulioupata,kwa ushauri zaidi tafuta kampuni za kisheria ujue wapi na hatua gani za kuanzia
 
Hao wameisha ziponda pesa hizo kwa mategemeo kuwa usumbufu utakufanya uzisamehe. Fatilia tu an pia dai fedha za usumbufu - hao ni wezi hawana lao - good luck
 
Fwata ushauri wa Gasper,fungua kesi ya madai mahakamani.na uwe na lawyer mzuri asiye na njaa maana wanaweza wakakuzunguka tena.
 
Fungua kesi ya madai kama milioni 20 hiv watapata akili wakati mwingine.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…