Sina budi kupongeza juhudi za serikali awamu ya kwanza na ya pili kwa maamuzi yao ya kuthamini michezo na kuweza kuhamasisha ujenzi wa viwanja vya michezo karibu katika mikoa yote.
Ujenzi huu ulitokana na michango ya wananchi wote bila kujali itikadi au kama ni mwanachama wa CCM au la,kwani kulikuwa na chama kimoja tu.
Mtindo wa ujenzi wa viwanja hivi ulikuwa kwa mfumo wa michango kama tulivyokuwa tunachangia ujenzi wa mashule ya kata wakati wa Mkapa na Jk.
Kutokana na nchi kuingia kwenye mfumo wa vyama vingi,CCM waliona vyema kujimilikisha viwanja hivyo na hasa kwa vile waliviita majina ya mfano CCM Kirumba.
Lakini kusema kweli, CCM imeshindwa kuvihudumia na sasa serikali inabidi ndiyo iingilie kati.Ijapo ni jambo gumu lakini kwa waungwana linawezekana. Kwani hivi vyama vya siasa ni vya watu wachache tu.Wananchi wengi hawajihusishi na vyama vya siasa.
Kwa mtu mzalendo, muungwana ataliona jambo hili. Raslimali za nchi, zisigawanwe kwa misingi ya makundi ya kisiasa au itikadi fulani,
Ili kila mtu afaidike sawa.
Ni muhimu kuvirudisha serikalini viwanja hivi sasa.Muda muafaka ndio huu.Na serikali inaweza kuvikabidhi kwa shirika la nyumba la taifa.
Hayo ni maoni yangu huru. Mimi sina itikadi ya chama chochote.Kuna watu humu huwa huwa wanafikiri kila mwananchi ni mfuasi wa chama fulani.Ninaongea kama mwanamichezo,ninayeona umuhimu wa serikali sasa kuwa na viwanja vyake yenyewe na Sio chama fulani cha siasa .
Ujenzi huu ulitokana na michango ya wananchi wote bila kujali itikadi au kama ni mwanachama wa CCM au la,kwani kulikuwa na chama kimoja tu.
Mtindo wa ujenzi wa viwanja hivi ulikuwa kwa mfumo wa michango kama tulivyokuwa tunachangia ujenzi wa mashule ya kata wakati wa Mkapa na Jk.
Kutokana na nchi kuingia kwenye mfumo wa vyama vingi,CCM waliona vyema kujimilikisha viwanja hivyo na hasa kwa vile waliviita majina ya mfano CCM Kirumba.
Lakini kusema kweli, CCM imeshindwa kuvihudumia na sasa serikali inabidi ndiyo iingilie kati.Ijapo ni jambo gumu lakini kwa waungwana linawezekana. Kwani hivi vyama vya siasa ni vya watu wachache tu.Wananchi wengi hawajihusishi na vyama vya siasa.
Kwa mtu mzalendo, muungwana ataliona jambo hili. Raslimali za nchi, zisigawanwe kwa misingi ya makundi ya kisiasa au itikadi fulani,
Ili kila mtu afaidike sawa.
Ni muhimu kuvirudisha serikalini viwanja hivi sasa.Muda muafaka ndio huu.Na serikali inaweza kuvikabidhi kwa shirika la nyumba la taifa.
Hayo ni maoni yangu huru. Mimi sina itikadi ya chama chochote.Kuna watu humu huwa huwa wanafikiri kila mwananchi ni mfuasi wa chama fulani.Ninaongea kama mwanamichezo,ninayeona umuhimu wa serikali sasa kuwa na viwanja vyake yenyewe na Sio chama fulani cha siasa .