OLS
JF-Expert Member
- Oct 12, 2019
- 426
- 685
Katika ulimwengu tulionao na kwa namna ya maisha tunayoishi ni wazi kuwa tuna muda finyu wa kujisomea mambo yenye hoja za msingi. Hali hii ni tatizo lakini kila jamii imejitahidi kutumia Sanaa na teknolojia kiujumla ili kuhakikisha kwamba watu wanapata mambo ambayo wangeyapata vitabuni.
Kupitia teknolojia, na kujua kuwa watu wana muda finyu wa kusoma, siku hizi imeanza mifumo ya kuweka vitabu katika mfumo wa video au sauti ili mtu aeze kusikiliza yote yaliyoandikwa kwenye kitabu huku akiendelea na shughuli nyingine
Uandishi wa vitabu ni mzuri lakini audio books zinafeli kwenye eneo la kushindwa kuwa na sanaa katika usomaji. Hapa ndipo inpoingia nafasi ya ushairi wa kuongea, ambayo kwa historia mashairi haya yalikuja ili kuwafanya watu wapate ujumbe kwa uzito wa ujumbe utolewayo, lakini pia mtu avutiwe na aburudike kusikia.
Ushairi wa kuongea, unaandikwa kwa uzito mkubwa hoja na maoni ambao sio lazima kufuata vina, kuwa na kiitikio nk, ila huwa na midundo ili kuwa na radha katika ghani zake.
Msanii wa Marekani Prince Ea, amewahi kueleza mafanikio yake mara baada kuamua kuachana na muziki wakufokafoka na kuingia kwenye mashairi akiwa inspire na ku-motivate watu wenye mambo tofauti tofauti
Pia yuko mtu mwenye PhD, Dr Cornel West ambaye naye anafanya spoken word poetry kwa nchini Marekani. Wasanii wa spoken word poetry wapo wengi kwa nchi zilizoendelea kuliko nchi za Afrika,
Tukijilinganisha na wenzetu wakenya sisi tuna wasanii wachache zaidi, wakiongozwa na bwana Mrisho Mpoto, Yupo bwana Justine Kakoko ambaye ana album mbili za ushairi, Uafrika ni Wajibu, na Duniani nyumbani. Yupo mwanadada Zuhura the lioness ambaye ana album ya Love blooms. Pia Male Hanzi amefanya mashairi kadhaa kwenye album yake ya hip hop alikuwa na track mbili za ushairi wa kuongea, Sababu ni moja na Kijiji cha kuku
Pia yupo Hellen Burugu ambaye ametamalaki Youtube kwa ngoma zake za ushairi wa kuongea. Pamoja na Amos Mwijonge
Ushairi wa kuongea unajali zaidi ujumbe kuliko vina, aina hii ya ushairi ni tofauti na ngonjera ambayo mara nyingi una namna moja ya ghani pia naziona ngonjera kama tambo za majigambo.
Katika huu ulimwengu ambao watu tuna matatizo mengi na tunahitaji faraja, lakini hatuna muda wa kusoma vitabu vya self help kutokana na ufinyu wa muda basi ni vyema kusikiliza mashairi kupata ujumbe ambao unaweza kuwa ni faraja au kupata hoja zinazoweza kuibua kiu ya kufahamu vitu ambavyo washairi wanaweza kuwa wamevizungumza katika kazi zao.
Teknolojia siku zote imekuwa msaada mkubwa kwenye kufanya maarifa yamfikie mwanaamu, tangu ugunduzi wa maandishi, ungunduzi wa wino, karatasi, printing press, computers na mambo mengine ambayo hufanya mtu kupata taarifa au maarifa
Signed: Oedipus
=====
Justine Kakoko
Zuhura
Malle Hanzi
Hellen Bulugu
Amosi Mwijonge
Kupitia teknolojia, na kujua kuwa watu wana muda finyu wa kusoma, siku hizi imeanza mifumo ya kuweka vitabu katika mfumo wa video au sauti ili mtu aeze kusikiliza yote yaliyoandikwa kwenye kitabu huku akiendelea na shughuli nyingine
Uandishi wa vitabu ni mzuri lakini audio books zinafeli kwenye eneo la kushindwa kuwa na sanaa katika usomaji. Hapa ndipo inpoingia nafasi ya ushairi wa kuongea, ambayo kwa historia mashairi haya yalikuja ili kuwafanya watu wapate ujumbe kwa uzito wa ujumbe utolewayo, lakini pia mtu avutiwe na aburudike kusikia.
Ushairi wa kuongea, unaandikwa kwa uzito mkubwa hoja na maoni ambao sio lazima kufuata vina, kuwa na kiitikio nk, ila huwa na midundo ili kuwa na radha katika ghani zake.
Msanii wa Marekani Prince Ea, amewahi kueleza mafanikio yake mara baada kuamua kuachana na muziki wakufokafoka na kuingia kwenye mashairi akiwa inspire na ku-motivate watu wenye mambo tofauti tofauti
Pia yuko mtu mwenye PhD, Dr Cornel West ambaye naye anafanya spoken word poetry kwa nchini Marekani. Wasanii wa spoken word poetry wapo wengi kwa nchi zilizoendelea kuliko nchi za Afrika,
Tukijilinganisha na wenzetu wakenya sisi tuna wasanii wachache zaidi, wakiongozwa na bwana Mrisho Mpoto, Yupo bwana Justine Kakoko ambaye ana album mbili za ushairi, Uafrika ni Wajibu, na Duniani nyumbani. Yupo mwanadada Zuhura the lioness ambaye ana album ya Love blooms. Pia Male Hanzi amefanya mashairi kadhaa kwenye album yake ya hip hop alikuwa na track mbili za ushairi wa kuongea, Sababu ni moja na Kijiji cha kuku
Pia yupo Hellen Burugu ambaye ametamalaki Youtube kwa ngoma zake za ushairi wa kuongea. Pamoja na Amos Mwijonge
Ushairi wa kuongea unajali zaidi ujumbe kuliko vina, aina hii ya ushairi ni tofauti na ngonjera ambayo mara nyingi una namna moja ya ghani pia naziona ngonjera kama tambo za majigambo.
Katika huu ulimwengu ambao watu tuna matatizo mengi na tunahitaji faraja, lakini hatuna muda wa kusoma vitabu vya self help kutokana na ufinyu wa muda basi ni vyema kusikiliza mashairi kupata ujumbe ambao unaweza kuwa ni faraja au kupata hoja zinazoweza kuibua kiu ya kufahamu vitu ambavyo washairi wanaweza kuwa wamevizungumza katika kazi zao.
Teknolojia siku zote imekuwa msaada mkubwa kwenye kufanya maarifa yamfikie mwanaamu, tangu ugunduzi wa maandishi, ungunduzi wa wino, karatasi, printing press, computers na mambo mengine ambayo hufanya mtu kupata taarifa au maarifa
Signed: Oedipus
=====
Justine Kakoko
Zuhura
Malle Hanzi
Hellen Bulugu
Amosi Mwijonge