Mkalukungone mwamba
JF-Expert Member
- Aug 29, 2022
- 862
- 1,755
Wanajukwaa Kwema!
Siku zinahesabika kuelekea uchaguzi wa serikali za mitaa ambao unatarajiwa kufanyika November 27 mwaka huu nchini kote.
Sasa swali la kujiuliza vipi muamko wa Wanawake wa vijijini kushiriki katika kuwania nafasi hizo ambapo mara zote kumekuwa na muhamko mdogo sana wa kuthubutu kuchukua fomu ndani ya vyama vyao vya kisiasa na kwenda kusimama kwenye majukwaa na kunadi sera zao mbele ya wananchi ili wapate nafasi za uongozi.
Ukizidi kuangalia kiujumla wanawake wamekuwa na muitikio mdogo sana kuwania nafasi mbalimbali za uongozi na wengine wakifika mbali na dhana potofu kuwa wanawake awana uwezo wa kuwa viongozi bora. Jambo ambalo binafsi naona si lakweli.
Ukitazama uthubutu kwenye uduchu wa wanawake wa mjini wamekuwa kidogo wanajitokeza na kuleta ushindani mkubwa kwa wanaume katika kugombea nafasi za uongozi wa taifa au ndani ya chama chake cha siasa ukilanganisha na wanawake wa vijijini ambao wamekuwa waoga na mfumo dume ambao umeendelea kutumika zaidi baadhi ya maeneo ya vijijini.
Sasa ni wakati sahihi kwa wanawake wa maeneo ya vijijini wenye uwezo na wenye kukidhi vigezo vya ugombea waanze mchakato sasa wakwenda kuchukua fomu za kuwania nafasi za uongozi katika uchaguzi wa serikali za mitaa.
Lakini naona pia Vyombo vya habari vinaweza kusaidia kuleta uhamasishaji kwa kuonyesha simulizi za wanawake waliofanikiwa, kutoa habari za motisha na fursa kwa wanawake wa vijijini. Matumizi ya redio za kijamii na mitandao ya kijamii vinaweza kufanikisha uhamasishaji huu.
Vipi na wewe mdau unamaoni gani kwenye hili?
Siku zinahesabika kuelekea uchaguzi wa serikali za mitaa ambao unatarajiwa kufanyika November 27 mwaka huu nchini kote.
Sasa swali la kujiuliza vipi muamko wa Wanawake wa vijijini kushiriki katika kuwania nafasi hizo ambapo mara zote kumekuwa na muhamko mdogo sana wa kuthubutu kuchukua fomu ndani ya vyama vyao vya kisiasa na kwenda kusimama kwenye majukwaa na kunadi sera zao mbele ya wananchi ili wapate nafasi za uongozi.
Ukizidi kuangalia kiujumla wanawake wamekuwa na muitikio mdogo sana kuwania nafasi mbalimbali za uongozi na wengine wakifika mbali na dhana potofu kuwa wanawake awana uwezo wa kuwa viongozi bora. Jambo ambalo binafsi naona si lakweli.
Ukitazama uthubutu kwenye uduchu wa wanawake wa mjini wamekuwa kidogo wanajitokeza na kuleta ushindani mkubwa kwa wanaume katika kugombea nafasi za uongozi wa taifa au ndani ya chama chake cha siasa ukilanganisha na wanawake wa vijijini ambao wamekuwa waoga na mfumo dume ambao umeendelea kutumika zaidi baadhi ya maeneo ya vijijini.
Sasa ni wakati sahihi kwa wanawake wa maeneo ya vijijini wenye uwezo na wenye kukidhi vigezo vya ugombea waanze mchakato sasa wakwenda kuchukua fomu za kuwania nafasi za uongozi katika uchaguzi wa serikali za mitaa.
Lakini naona pia Vyombo vya habari vinaweza kusaidia kuleta uhamasishaji kwa kuonyesha simulizi za wanawake waliofanikiwa, kutoa habari za motisha na fursa kwa wanawake wa vijijini. Matumizi ya redio za kijamii na mitandao ya kijamii vinaweza kufanikisha uhamasishaji huu.
Vipi na wewe mdau unamaoni gani kwenye hili?