Nafasi za kazi 9,483 za Kada za Afya

Nafasi za kazi 9,483 za Kada za Afya

OR TAMISEMI

Ministry
Joined
Jul 3, 2024
Posts
20
Reaction score
93

Kumb.Na.JA.9/259/01/B/ 11


Katibu wa Sekretarieti ya Ajira Katika Utumishi wa Umma kwa niaba ya Sekretarieti za Mikoa na Mamlaka ya Serikali za Mitaa inakaribisha maombi ya kazi kutoka kwa Watanzania wenye sifa na uwezo wa kujaza nafasi 9,483 kama ilivyoainishwa katika tangazo hili.​

Maeneo ya Kazi:

  • Arusha: 9
  • Dar es Salaam: 3
  • Geita: 38
  • Iringa: 26
  • Kagera: 18
  • Katavi: 32
  • Kigoma: 29
  • Kilimanjaro: 25
  • Lindi: 19
  • Manyara: 15
  • Mara: 24
  • Mbeya: 28
  • Morogoro: 18
  • Mtwara: 49
  • Mwanza: 17
  • Njombe: 18
  • Pwani: 18
  • Rukwa: 26
  • Ruvuma: 23
  • Shinyanga: 28
  • Simiyu: 33
  • Singida: 24
  • Songwe: 24
  • Tabora: 39
  • Tanga: 53

MASHARTI YA JUMLA.​

  1. Waombaji wote wawe ni Raia wa Tanzania na wenye umri usiozidi miaka 45 isipokuwa kwa wale tu walioko kazini serikalini;​
  2. Waombaji wenye ulemavu wanahamasishwa kutuma maombi na wanapaswa kuainisha kwenye mfumo wa kuombea ajira ulemavu walionao kwa ajili ya taarifa kwa Sekretarieti ya Ajira katika Utumishi wa Umma;​
  3. Waombaji wote waambatishe cheti cha kuzaliwa kilichothibitishwa na Mwanasheria/Wakili.​
  4. Waombaji ambao tayari ni watumishi wa Umma na wamejipatia sifa za kuingilia katika kada tofauti na walizonazo, wapitishe barua zao za maombi ya nafasi za kazikwa Waajiri wao na Waajiri wajiridhishe ipasavyo.​
  5. Waombaji waambatishe maelezo binafsi yanayojitosheleza (Detailed C.V) yenye anwani na namba za simu za kuaminika pamoja na majina yawadhamini (referees) watatu wa kuaminika.​
  6. Maombi yote yaambatane na vyeti vya taaluma, maelezo, nakala za vyeti vilivyothibitishwa na Mwanasheria/Wakili ambavyo ni vyeti vya kuzaliwa, kidato cha Nne, kidato cha Sita kwa wale waliofikia kiwango hicho, na vyeti vya kuhitimu mafunzo mbalimbali kwa kuzingatia sifa za kazi husika.
    • Postgraduate/Degree/Advanced Diploma/Diploma/Certificates.
      • Cheti cha mtihani wa kidato cha IV na VI
      • Computer Certificate
      • Vyeti vya kitaaluma (Professional certificates from respective boards)
  7. “Testmonials”, “Provisional Results”, “Statement of results”, hati matokeo zakidato cha nne na sita (FORM IV AND FORM VI RESULTS SLIPS) HAVITAKUBALIWA.
  8. Waombaji waliosoma nje ya Tanzania wahakikishe vyeti vyao vimehakikiwa na kuidhinishwa na Mamlaka husika (TCU, NECTA na NACTE).​
  9. Waombaji waliostaafishwa katika Utumishi wa Umma hawaruhusiwi kuomba isipokuwa kama wana kibali cha Katibu Mkuu Kiongozi.​
  10. Waombaji kazi ambao tayari ni waajiriwa katika nafasi za kuingilia walioko katika Utumishi wa Umma wasiombe na wanatakiwa kuzingatia maelekezo yaliyo katika Waraka Na CAC. 45/257/01/D/140 wa tarehe 30 Novemba, 2010.
  11. Uwasilishaji wa taarifa na sifa za kughushi wahusika watachukuliwa hatua za kisheria.​
  12. Mwisho wa kutuma maombi ya kazi ni tarehe 20 Julai, 2024

MUHIMU: Kumbuka kuambatisha barua yako ya maombi ya kazi iliyosainiwa pamojana vyeti vya elimu, anuani ya barua hiyo ielekezwe kwa;​

KATIBU,​
OFISI YA RAIS,​
SEKRETARIETI YA AJIRA KATIKA UTUMISHI WA UMMA,​
S. L. P. 2320, DODOMA.​

Maombi yote yatumwe kwenye mfumo wa kielektroniki wa Ajira(Recruitment Portal) kupitia anuani ifuatayo;
(Anuani hii pia inapatikana kwenye tovuti ya Sektretarieti ya Ajira kwa kuingia sehemu iliyoandikwa‘Recruitment Portal’)

Maombi yatakayowasilishwa nje ya utaratibu ulioainishwa katika tangazo hili HAYATAFIKIRIWA.


Kutuma maombi, tembelea: Public Service Recruitment Secretariat website.
 

Attachments

IMG-20240707-WA0005.jpg
 
Mambo ya ku certify vyeti ya Nini? Ondoeni hicho kipengele maana mmewatengenezea ulaji tu mawakili/wanasheria. Washaurini hao Sekretarieti katika utumishi wa umma waondoe hicho kipengele Cha ku certify vyeti. Yaani maisha ya 2013 Bado tunayaishi kweli??
Katibu wa Sekretarieti ya Ajira Katika Utumishi wa Umma kwa niaba ya Sekretarieti za Mikoa na Mamlaka ya Serikali za Mitaa inakaribisha maombi ya kazi kutoka kwa Watanzania wenye sifa na uwezo wa kujaza nafasi 9483 kama ilivyoainishwa katika tangazo hili.

 
Mbona kila nikifungua post za daktari daraja la 11,
qualifications zinataka wa shahada TU na tangazo limeruhusu adi wa stashahada kuomba Nini shida hapo???????
 
Mbona kila nikifungua post za daktari daraja la 11,
qualifications zinataka was shahada TU na tangazo limerihusu adi wa stashahada kuomba Nini shida hapo???????
Mbona zipo mkuu endelea kwenye page nyingnee usiishie tuu kwenye page ya mwanzo
 
Mbona kila nikifungua post za daktari daraja la 11,
qualifications zinataka wa shahada TU na tangazo limeruhusu adi wa stashahada kuomba Nini shida hapo???????
Daktari ni mwenye Shahada.
Astashahada ni Afisa Tabibu Msaidizi. Soma maelekezo vizuri.
 
Mambo ya ku certify vyeti ya Nini? Ondoeni hicho kipengele maana mmewatengenezea ulaji tu mawakili/wanasheria. Washaurini hao Sekretarieti katika utumishi wa umma waondoe hicho kipengele Cha ku certify vyeti. Yaani maisha ya 2013 Bado tunayaishi kweli??
Sasa wanasheria wale wapi nahuku ajira hamna
 
Mambo ya ku certify vyeti ya Nini? Ondoeni hicho kipengele maana mmewatengenezea ulaji tu mawakili/wanasheria. Washaurini hao Sekretarieti katika utumishi wa umma waondoe hicho kipengele Cha ku certify vyeti. Yaani maisha ya 2013 Bado tunayaishi kweli??
Nenda mahakamani upate certification ya vyeti, not necessarylily kwa mawakili. Any officer with the power to administer notaries and commission for oaths

 
Back
Top Bottom