Salaam wana JF
Naomba kuulizia kuhusu hizi nafasi za walioomba kujiunga na vyuo vya ualimu (Certificate level) kwa waliomaliza form IV. Nimejaribu kuangalia threads zingine naona ni nafasi za Stashahada tu zimetoka, lakini hawa walioomba kwa ngazi ya Certificate kwa kweli sijaona. Nafasi nilimuombea mdogo wangu hivyo namsaidia kufanya follow up.
Natanguliza shukurani.
CC. lusungo
Mkuu kwa sasa hakuna certificate ya ualimu Wa msingi.....
Wameupdate mfumo hivyo now wale Wa certificate watasoma diploma ya kawaida miaka 2 na wale Wa diploma (form six) watasoma advance diploma...
Hivyo wale wote walioaply ualimu ngazi ya cheti automatically wamepelekwa kwenye stashada ya ualimu Wa nsingi..awali...na michezo...
Pia kuna suala la half combination kwa form four wenye ufaulu Wa sayansi kusomea advance diploma kwa miaka 3 japo halijawa clear....
Pole mkuu kwa usumbufu but ndo serikali yetu hiyo ilipaswa wadau mjulishwe na kupewa elimu ya kina ili msihangaike....
Nashukuru sana kwa ufafanuzi wako mkuu lusungo, sasa huko ambako wamepelekwa (Stashahada ya elimu ya msingi, awali na michezo) nawezaje kuona majina mkuu maana nimecheki www.moe.go.tz sijaona update yoyote kule.