ipogolo
JF-Expert Member
- Aug 15, 2011
- 6,280
- 5,979
Katika gazeti la Mwananchi la tarehe 12 Agosti 2013, Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi walitoa tangazo la nafasi za mafunzo maalumu ya ualimu tarajali ngazi ya stashahada(diploma) katika masomo ya sayansi na hisabati.
Mwisho wa kupokea maombi ilikuwa tarehe 20 Agosti 2013.
Kinachoshangaza ni kuwa waombaji wanaoishi Dar es Salaam , na mikoa jirani wapeleke barua zao kwa mkono na kuweka katika kisanduku kilichopo mapokezi.
Gharama ya kupanda basi kutoka mikoa jirani hadi dsm kwa watoto wa kawaida maskini huo sio unyanyasaji kiuchumi kisaikolojia na kijamii?
Kwani Shirika la Posta Limefungwa na halisafirishi barua ambapo ninaamini gharama haitazidi shs 1000/?.
Wizara niwaombe kwa niaba ya watanzania makabwela mtufikirie kuturuhusu kutuma maombi kwa njia ya posta.
Mwisho wa kupokea maombi ilikuwa tarehe 20 Agosti 2013.
Kinachoshangaza ni kuwa waombaji wanaoishi Dar es Salaam , na mikoa jirani wapeleke barua zao kwa mkono na kuweka katika kisanduku kilichopo mapokezi.
Gharama ya kupanda basi kutoka mikoa jirani hadi dsm kwa watoto wa kawaida maskini huo sio unyanyasaji kiuchumi kisaikolojia na kijamii?
Kwani Shirika la Posta Limefungwa na halisafirishi barua ambapo ninaamini gharama haitazidi shs 1000/?.
Wizara niwaombe kwa niaba ya watanzania makabwela mtufikirie kuturuhusu kutuma maombi kwa njia ya posta.