Nafikiri ni wakati wa familia za viongozi wa upinzani kudai Katiba Mpya

kipara kipya

JF-Expert Member
Joined
May 2, 2016
Posts
18,833
Reaction score
23,276
Kipindi kirefu viongozi wa upinzani wameshupaza shingo kuhamasisha uhuni wa maandamano dhidi ya serikali halali ya nchi yetu.

Nafikiri muda umefika sasa na najua viongozi wote wana watoto wakubwa tu wa kuweza kutoka barabarani ingekuwa vyema kwa kuwa chadema na wanaharakati uchwara wapo kwenye kushinikiza katiba mpya,hiyo ni njia bora kuliko yale makongamano.

Wangeungana na kutoa watoto,wake,waume na mama zao,
Wajitokeze kwa wingi wamsaidie mzee wao aliyepo mahabusu.

Sisi hatuna muda wa kupoteza zaidi ya kutafuta dona la wanetu kuliko kwenda kupigania tumbo la mwingine ambaye akipata ruzuku wala hatujali.

Huu ni ushauri kila mmoja ahamasishe familia yake
1.Mbowe
2.Lissu
3.Lema
4.Msigwa
5.Heche
Najua mnyika yeye ni mstaarabu hapendi hamasisha uhuni wala hana watoto wakubwa.
Zitto kabwe na James Mbatia mkiwatoa familia zenu tutaunga mkono bila mashariti!
Nimeandika hapa baada ya kuona watu wengi wapo jela wamepata ulemavu halafu walio wahamasisha wamekimbia kujificha nje na familia zao wala hazijadhurika!
 
Sio bure, umerogwa.
 
Hii imekaa vizuri sana
 

Akili za mazuzu wa ccm ni shida
 
Hili ni swala binafsi haihitaji usimamizi wa mtu mwingine

Mbowe akihamasisha hua haitengi familia yake hivyo wakielewa watashiriki
 
Wenzako wamejifungia wanaandika mashitaka ya UGAIDI upya wewe unazurura zurura humu JF utalipwaje sasa.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…