mshamba_mwingine
JF-Expert Member
- Jul 23, 2023
- 1,057
- 4,145
Leo nimekutana na hii makala mtandaoni, imenishtua na kunishangaza sana.
Mwanaume mmoja huko india ameamua kuacha kazi yake katika taasisi kubwa sana ya goldman sachs yenye mshahara mzuri, na kuwa baba wa nyumbani, ili ampe mke wake urahisi wa kupanda cheo kazini.
Anadai kwamba wanawake wengi wanakosa vyeo vikubwa kwasababu ya kujikita kwenye malezi ya watoto, hivyo wanaume wanatakiwa wajitolee zaidi kubaki nyumbani.
Vile vile anagawana na mke wake majukumu ya malezi, pale mke anapokuwa nyumbani....
Na pia ameamua(na kuridhika) kuishi kupitia mshahara wa mkewe, pamoja na akiba yao ya pamoja.
Nawaza, kama kuna wanaume wanaothubutu kufanya jambo kama hili, na likashamiri, mustakhabali wa wanaume kwenye mahusiano utakuwaje?
Wanaume tutafafanuliwa katika misingi ipi?
Hii ni sawa kweli?
Nimechanganyikiwa.
Mwanaume mmoja huko india ameamua kuacha kazi yake katika taasisi kubwa sana ya goldman sachs yenye mshahara mzuri, na kuwa baba wa nyumbani, ili ampe mke wake urahisi wa kupanda cheo kazini.
Anadai kwamba wanawake wengi wanakosa vyeo vikubwa kwasababu ya kujikita kwenye malezi ya watoto, hivyo wanaume wanatakiwa wajitolee zaidi kubaki nyumbani.
Vile vile anagawana na mke wake majukumu ya malezi, pale mke anapokuwa nyumbani....
Na pia ameamua(na kuridhika) kuishi kupitia mshahara wa mkewe, pamoja na akiba yao ya pamoja.
Nawaza, kama kuna wanaume wanaothubutu kufanya jambo kama hili, na likashamiri, mustakhabali wa wanaume kwenye mahusiano utakuwaje?
Wanaume tutafafanuliwa katika misingi ipi?
Hii ni sawa kweli?
Nimechanganyikiwa.