Nafuga Paka, nisaidieni......

Nafuga Paka, nisaidieni......

Nojo Wemah

Member
Joined
Aug 9, 2017
Posts
21
Reaction score
19
Anaitwa Maui, nilimchukua akiwa mdogo kabisaa. Kwa kipindi cha ukuaji hapo nyuma kulikuwa na watoto wa jirani walikuwa wakicheza nae na mda mwingine walikuwa wakicheza nae vibaya kwa kumpiga hali hiyo imemfanya Maui kuwa mkorofi hasa akiwa na njaa. Kuna wakati mwingine bila sababu tu anaweza akakuparua (hii hutokea mara chache chache). Nashindwa nini nifanye ili aache hii tabia ya kuparua.
Maui anatabia ingine ya kubagua msosi ambayo ni tofauti Kwa paka wengine ambao nimekuwa nikiona wanakula vyakula vya kawaida kabisa vinavyoliwa na watu wanao wafuga, sijui ni kwa nini yeye anabagua msosi, miezi miwili nyuma nilimpatia dawa ya minyoo nikidhani labda huenda alikuwa na minyoo iliyomfanya asile chakula ambacho sie tunakula lakini pamoja na kumpatia dawa ya minyoo bado Maui aliendelea na mtindo wake wa kubagua msosi. Ili ale yeye muekee samaki au nyama tofauti na hapo ali kabisa atunusanusa hapo kisha ataacha. NIFANYE NINI ILI MAUI AWE ANAKULA MSOSI BILA KUBAGUA, MBONA WENGINE HAWABAGUI?? NIJUZENIIII....
 
nilitaka kuuliza ni season ya ngapi kumbe siyo tamthiliya
 
Maui!! Umenikumbusha ile animation movie ya Moana! "Maui,mauiii ur so amaizinggg"
 
mafumbo yasiyo na faida yoyote kwa msomaji!
 
Kuwahudumia hao viumbe ni gharama sana sisi tunawalea kiswazi Swazi tu,mpeleke hospital huyo anaweza kuwa na kichaa cha mbwa
 
Wa kwangu nimempa kazi ya kulinda Pumba ,asipokamata panya huko hana option ya kula ...
Nakushauri wa kwako muwekee oda ya samaki
 
Kuna kipi huwa kinarushwa discovery family kinaitwa my cat from hell dah nngekushauri uangalie maana hapo kuna jamaa ana badilisha tabia ya paka na kua nzuri kabisa ambayo paka anakua very friendly
 
maui paka wa dar anakula nyama na samaki tu.
Hebu mpitishe neutral siki 3 afu mpe ugal uone kama atachomoa
Hili ndo jibu sahihi, hata mimi ninaye alitaka kuleta style hizi aiseee nikawaambia vijana wasihangaike naye waweke chochote asipokula wanamuacha njaa ikimuuma atakula paka wangu habagui chakula ugali, wali, mkate, mihogo anakula aiseee maake anajua asipokula ni njaa tu ndo atapambana nayo
 
Back
Top Bottom