Nafungua duka la nguo leo, naomba msaada

Nafungua duka la nguo leo, naomba msaada

kancher

JF-Expert Member
Joined
Dec 19, 2015
Posts
469
Reaction score
467
Habari zenu waungwana,
Natarajia kufungua duka la nguo siku ya leo mkoa wa Manyara, wilaya ya Babati ( Magugu).

Naomba msaada wa yafuatayo:-
Natarajia kwenda Dar wiki ijayo, mwenye connection na wauzaji wa jeans na track kwa jinsia zotekwà bei ya jumla.

Pia mwenye connection ya wauzaji wa viatu vya special vya kisasa kwa jinsia zote bei ya jumla pia.

Pia connection kwa wauzaji wa nguo na viatu vya mtumba grad one, lakini hizi tachukua kwa awamu ya pili baada ya kurudi tena kuchukua mzigo.

Pia naomba connection ya usafiri mimi pamoja na mizigo, au ushauri njia ipi ni nzuri kwa kusafirisha mizigo yangu kwa usalama na nafuu.

Ratiba yangu natarajia kuondoka alhamisi tar 20 usiku na kugeuka kurudi huku tar 23 jumapil mwezi huu wa August.

Nitashukuru kwa atakayenipa ushirikiano [emoji122]
 
Usha Fanya Market research hapo Magugu kwanza kujua kuna Maduka kaisi gani yanayo uza vitu kama unavyo taka kuuza? na biashara ikoje? Make Nguo sio kama chakula kwamba lazima mtu awe nayo
Huyu hajajiandaa kwa lolote, kwa mawazo yangu. Umeona hayo aliyouliza? Hivi inakuingia kwenye akili mtu anayesema anafungua duka la nguo leo kuuliza hayo aliyouliza?

Hayo ndiyo mambo aliyotakiwa kufanyia utafiti hata kabla ya kufanya uamuzi wa kufungua duka la nguo. Tanzania hizi biashara nyingi ndogo hufa kwa sababu hii.

Mtu akitembea mitaani, akiona biashara yoyote iliyopendeza macho yake anakimbilia kwenda kuifanya bila utafiti wowote.
 
Kwa connections za wauzaji wa jeans na raba tshirt kali ntakusaidia, lkn pia km hautojali naweza kuwa winga wako wa kariakoo, yani huna haja ya kusafiri safiri, kwakua mimi nipo dar na najua nguo zinazo trend kwa muda huo ntakuwa nakukusanyia na kukutumia ktk bus.

Hii itakusaidia kila siku kuwa na fashion mpya dukani kwako. Maana haitahitaji uwe na cash nyingi ili ufate mzigo, yani hata ukiwa na laki sita unaandika order.
 
Kwa connections za wauzaji wa jeans na raba tshirt kali ntakusaidia, lkn pia km hautojali naweza kuwa winga wako wa kariakoo, yani huna haja ya kusafiri safiri, kwakua mimi nipo dar na najua nguo zinazo trend kwa muda huo ntakuwa nakukusanyia na kukutumia ktk bus. Hii itakusaidia kila siku kuwa na fashion mpya dukani kwako. Maana haitahitaji uwe na cash nyingi ili ufate mzigo, yani hata ukiwa na laki sita unaandika order.
Asante, tatumia hii njia lakini kwa mara ya kwanza lazima nifike kwanza nitengeneze connection za address zinazoeleweka. Ili inapotokea tatizo niweze kujua naanzia wapi.
 
jitahidi tafuta wafanyabiashara wanaotokea huko kwenu wakuongoze na kukupa ramani yote wapi wanafanyia shopping, wapi hupakilia mizigo yao huku mitandaoni hakuko salama utajiconnect na watu wasio na nia njema ukabananishwe kweny kona mtaji uende, otherwise nakutakia kila la kher mkuu
 
Nd
Asante, tatumia hii njia lakini kwa mara ya kwanza lazima nifike kwanza nitengeneze connection za address zinazoeleweka. Ili inapotokea tatizo niweze kujua naanzia wapi.
Ndiyo ni lazima ufike angalau mara mbili kisha mambo mengine yatafuata.
 
jitahidi tafuta wafanyabiashara wanaotokea huko kwenu wakuongoze na kukupa ramani yote wapi wanafanyia shopping, wapi hupakilia mizigo yao huku mitandaoni hakuko salama utajiconnect na watu wasio na nia njema ukabananishwe kweny kona mtaji uende, otherwise nakutakia kila la kher mkuu
Asante mkuu, nimefanyia kazi pia wazo hili,, huku nilikuwa natàkà kupata option nyinginw zaidi.
Nipo makini tachukua tahadhari pia. Na kwa dàr mimi sio mgen sana nimeishi zaidi ya miaka 7.
 
Kwa connections za wauzaji wa jeans na raba tshirt kali ntakusaidia, lkn pia km hautojali naweza kuwa winga wako wa kariakoo, yani huna haja ya kusafiri safiri, kwakua mimi nipo dar na najua nguo zinazo trend kwa muda huo ntakuwa nakukusanyia na kukutumia ktk bus. Hii itakusaidia kila siku kuwa na fashion mpya dukani kwako. Maana haitahitaji uwe na cash nyingi ili ufate mzigo, yani hata ukiwa na laki sita unaandika order.
Mkuu hebu iweke sawa hii, malipo yanakuwaje? utatumiwa fedha kabla ya mzigo kufika au baada ya mzigo kufika
 
Usha Fanya Market research hapo Magugu kwanza kujua kuna Maduka kaisi gani yanayo uza vitu kama unavyo taka kuuza? na biashara ikoje? Make Nguo sio kama chakula kwamba lazima mtu awe nayo
Yes nimefanya market research kwa muda ktk maeneo ya karibu na ninayoishi, na eneo hilo kwa malengo yangu niliyojiwekea nimelizishwa nalo. Naomba na Mingu pia anisaidie.
 
Huyu hajajiandaa kwa lolote, kwa mawazo yangu. Umeona hayo aliyouliza? Hivi inakuingia kwenye akili mtu anayesema anafungua duka la nguo leo kuuliza hayo aliyouliza? Hayo ndiyo mambo aliyotakiwa kufanyia utafiti hata kabla ya kufanya uamuzi wa kufungua duka la nguo. Tanzania hizi biashara nyingi ndogo hufa kwa sababu hii. Mtu akitembea mitaani, akiona biashara yoyote iliyopendeza macho yake anakimbilia kwenda kuifanya bila utafiti wowote.
Umenisimanga sana kwasababu sijaeleza kiundani,, lkn ofisi nimefungua na nimeanza kufanya kwa kiwango cha chini. Na connection baadhi ninazo, huku nilihitaji kupanua mawazo zaidi kwasabu nataka kujitanua kitofauti kwa huku na kuongeza ubora wa kazi zangu.
 
Habari zenu waungwana,
Natarajia kufungua duka la nguo siku ya leo mkoa wa Manyara , wilaya ya Babati ( Magugu)

Naomba msaada wa yafuatayo:-
Natarajia kwenda Dar wiki ijayo, mwenye connection na wauzaji wa jeans na track kwa jinsia zotekwà bei ya jumla.

Pia mwenye connection ya wauzaji wa viatu vya special vya kisasa kwa jinsia zote bei ya jumla pia.

Pia connection kwa wauzaji wa nguo na viatu vya mtumba grad one, lakini hizi tachukua kwa awamu ya pili baada ya kurudi tena kuchukua mzigo.

Pia naomba connection ya usafiri mimi pamoja na mizigo, au ushauri njia ipi ni nzuri kwa kusafirisha mizigo yangu kwa usalama na nafuu.

Ratiba yangu natarajia kuondoka alhamisi tar 20 usiku na kugeuka kurudi huku tar 23 jumapil mwezi huu wa August.

Nitashukuru kwa atakayenipa ushirikiano [emoji122]
nicheki pm nikupe number
 
Back
Top Bottom